Uyahudi

From Wikipedia

"Magen David" au nyota ya Daudi ni ishara ya Uyahudi
"Magen David" au nyota ya Daudi ni ishara ya Uyahudi
Menora au tawafa ya mikono saba pamoja na yarmulke au kofia ya Kiyahudi ni pia ishara za imani
Menora au tawafa ya mikono saba pamoja na yarmulke au kofia ya Kiyahudi ni pia ishara za imani

Uyahudi ni kati ya dini za kale sana ya binadamu. Imani yake ni katika Mungu mmoja tu aliyeumba mbingu na dunia aliyeteua ukoo wa Ibrahimu kuwa taifa teule. Wafuasi wa Uyahudi huitwa "Wayahudi" kuna takriban milioni 13 -14 duniani.

Uyahudi ni pia jina la kihistoria la sehemu ya nchi ya Palestina au Israel.

Hata kama iadi ya Wayhudi ilikuwa ndogo muda wowote duniani imaniy ao ilikuwa na athira kubwa. Wataalamu wengine huuita "dini mama" ya Ukristo na Uislamu.

Kwa jumla kuna namna mbili za kuangalia Uyahudi: ama kama dini au kama taifa. Namna zote mbili huchanganyikiwa na kutumiwa pamoja mara kwa mara.

Kuna Wayahudi wanaojitazama raia wa nchi fulani na Uyahudi wao ni katika imani tu. Kuna Wayahudi wengine wanaosema ya kwamba hawafuati dini wala hawaamini lakini wanajisikia kuwa Wayahudi kwa sababu za ukoo na pia desturi za utamaduni wao.

[edit] Imani

Kuna namna mbalimbali katika imani ya Kiyahudi kama madhehebu. Mara nyingi kanuni 13 za mwalimu Myahudi Maimonides aliyeishi katika karne ya 12 hukubaliwa na Wayahudi wengi.

  1. Mungu alikubali kila kita anaendelea kuangalia umbaji wake.
  2. Mungu ni mmoja tu na hana kasoro wala kosa.
  3. Mungu hana mwili hafanani na kitu chochote duniani.
  4. Mungu alikuwepo daima ataendelea kuwepo milele.
  5. Sala zifanywe kwa Mungu pekee.
  6. Mafundisho ya manabii wa Kiyahudi ni ya kweli.
  7. Musa alikuwa nabii mkuu wa nyakati zote hakuna atakayemshinda.
  8. Mungu alimpa Musa torati.
  9. Torati haitabadilishwa na hapatakuwa na torati nyingine.
  10. Mungu anajua dhana na mawazo wa kila mtu.
  11. Mungu atawatuza wenye haki na kuwaadhibu waovu.
  12. Masiya atakuja.
  13. Wafu watafufuka.

[edit] Mitzvot - Amri

Kuna matendo fulani ambayo ni muhimu katika imani hii. Inaitwa mitzvot au amri. mitzvah ni amri ya Mungu kwa Wayahudi. Kuna amri 613 zinazojulikana kutoka torati. Sehemu ya amri hizi hazitekelezwi leo kwa sababu zinahusu hekalu ya Yerusalemu iliyoharibiwa mwaka 70 BK.

Amri kumi zina nafasi ya pekee kati ya amri zote.

Pamoja na amri hizi za torati kuna maelezo mapana katika Talmudi. Hata madai ya Talmudi mara nyingi zatajwa kama "mizvot". Ila tu ni tabia ya Uyahudi ya kwamba wataalamu hutofautiana juu ya maelezo haya mara kwa mara.

Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Uyahudi" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Uyahudi kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.