Hanoi
From Wikipedia
|
|
---|---|
![]() Barabara Le Thai To mjini Hanoi |
|
|
|
Mkoa | Hanoi |
Anwani ya kijiografia | 21°2'N, 105°51'E |
Kimo | 18 m juu ya UB |
Eneo | 921 km² |
Wakazi | 3.083.800 (2004) |
Msongamano wa watu | watu 3.348 kwa km² |
Simu | 84 (nchi), 4 (mji) |
Mahali | |
Hanoi (Kivietnam: Hà Nội; "mji kati ya mito") ni mji mkuu wa Vietnam mwenye wakazi zaidi ya milioni 3.
Mji uko kando la Mto Mwekundu katika delta ya mto huu takriban km 60 kabla ya mdomo wake.
[edit] Historia
Kati ya 1945 hadi 1976 ilikuwa mji mkuu wa Vietnam ya Kaskazini. Iliwahi kuwa mji mkuu wa sehemu kubwa ya Vietnam kati ya karne ya 11 hadi 1802 hadi uhamisho wa Kaisari kwenda Hue.
1873 Hanoi ilivamiwa na Ufaransa ikawa makao makuu ya koloni yake ya Indochina iliyounganisha Vietnam na Kambodia. Muundo wa mji wa leo umetokana na utawala wa Wafaransa waliopanga barabara pana na nyofu na mpango wa miraba lakini walibomoa sehemu kubwa ya mji wa kale.
Kati ya 1940 hadi 1945 Hanoi ilitawaliwa na Japani iliyoshiriki na utawala wa Kifaransa.
Tar. 2 Septemba 1945 rief Ho Chi Minh alitangaza mjini hanoi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Vietnam. Cheo cha mji mkuu wa nchi kikarudishwa kutoka Hue kuja Hanoi.
Kati 1946 hadi 1954 mji uliona mapigano makali ya Wafaransa na jeshi la ukombozi wa Viet Minh. Wakati wa vita ya Marekani katika Vietnam Hanoi iliona uharibifu kutokana na mabomu ya Marekani. Krismasi ya 1872 matani 40,000 za baruti yaitupwa Hanoi.
Tangu maungano ya Vietnam hanoi imekuwa mji mkuu wa nchi yote.
[edit] Uchumi
Leo hii hanoi ni mji wa viwanda ikiwa na nafasi ya pili baada ya Mji wa Ho Chi Minh (Saigon) katika kusini. Kuna viwanda vya machine, kemia, nguo ba bidhaa za ubao.
[edit] Picha za Hanoi
![]() |
Makala hiyo kuhusu "Hanoi" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri". Ikiwepo makala kuhusu Hanoi kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili. |