John Fisher
From Wikipedia
John Fisher (1469 – 22 Juni, 1535) alikuwa padre Mkatoliki kule Uingereza. Pia aliitwa John wa Rochester. Alimkataa mfalme Henry VIII aliyejitenga na Kanisa la kikatoliki. Kwa hiyo, John Fisher alifungwa ndani na baada ya kushtakiwa mahakamani aliuawa. Mwaka wa 1935 alitangazwa kuwa mtakatifu. Sikukuu yake ni 9 Julai.