Banjul
From Wikipedia
Banjul ni mji mkuu wa Gambia. Mji mwenyewe una wakazi 34,828 pekee lakini pamoja na mitaa ya nje ni zaidi ya nusu milioni.
Banjul iko kwenye kisiwa cha Mt. Mariamu (au: Kisiwa cha Banjul) mdomoni wa mto Gambia unapoishia katika Atlantiki.
[edit] Historia
Waingereza walianzisha mji mwaka 1816 BK kama kituo cha biashara na kituo cha kijeshi cha kukomesha biashara ya watumwa. Jina la mji lilikuwa "Bathurst" kufuatana na Henry Bathurst aliyekuwa waziri wa koloni wakati ule.
Mwaka 1965 Bathurst ilikuwa mji mkuu wa nchi huru ya Gambia. 1973 jina lilibadilishwa kuwa Banjul. Tarehe 22. Julai 1994 palikuwa na mapinduzi wa kijeshi lililoanzisha utawala wa Rais Jammeh. Geti ya mji wa "Arch 22" ilijengwa kama kumbukumbu ya mapinduzi haya.
[edit] Uchumi
Banjul ni kitovu cha utawala na biashara katika Gambia. Mawasiliano ndani ya nchi ni hasa kwa njia ya feri kwenye mto Gambia hadi mji wa Barra. Msingi wa uchumi ni kilimo, hasa karanga, nta, mawese na ngozi zinasafirishwa kutoka bandari ya Banjul. Banjul ina kiwanja cha ndege cha kimataifa.