Bibi Titi Mohammed

From Wikipedia

Bibi Titi Mohammed ni mmoja wa wanawake wa kwanza kushika nafasi za ubunge na uwaziri nchini Tanzaniana pia ni kati ya wanawake wa kwanza kujiunga na harakati za kugombea uhuru wa Tanganyika.

Mwaka 1969 Bibi Titi Mohammed alikamatwa na mwaka uliofuata alifikishwa mahakamani kwa kosa la kula njama ya kutaka kupindua serikali. Katika kesi hiyo, Bibi Titi alikuwa ni mwanamke pekee katika washtakiwa 7. Baada ya kesi hiyo kusikilizwa alipatikana na hatia na kuhumiwa kifungo cha maisha. Hata hivyo, mwaka 1972 alisamehewa na rais.