Wilhelm Conrad Röntgen
From Wikipedia
Wilhelm Conrad Röntgen (27 Machi, 1845 – 10 Februari, 1923) alikuwa mwanafizikia kutoka nchi ya Ujerumani. Hasa anajulikana kwa ugunduaji wa mionzi ya eksirei. Mwaka wa 1901 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fizikia.