Kaskazini-Magharibi (jimbo la Afrika Kusini)
From Wikipedia
![]() |
|
Eneo | 116 320 km² |
Wakazi (2001) | 3 669 349 |
Lugha | Kitswana (65.4%) Kiafrikaans (7.5%) Kixhosa (5.9%) Kisotho (5.7%) Kitsonga (4.7%) Kisepedi (4.2%) Kizulu (2.5%) KiNdebele (1.3%) Kiingereza (1.2%) |
Wakazi kimbari | Waafrika Weusi(91.5%) Wazungu(6.7%) Chotara(1.6%) Wenye Asili ya Asia (0.3%) |
Mji Mkuu | Mafikeng |
Waziri Mkuu | Edna Molewa (ANC) |
![]() |
Kaskazini-Magharibi ni jimbo la Afrika Kusini. Mji mkuu ni Mafikeng. Jimbo liliundwa baada ya mwisho wa siasa ya Apartheid kutokana na sehemu za majimbo ya awali ya Transvaal na Jimbo la Rasi pamoja na sehemu kubwa ya Bantustan ya Bophuthatswana.
[edit] Jiografia
Jimbo limepakana na nchi ya Botswana na majimbo yafuatayo ya Afrika Kusini:
Eneo lake ni 116,190 km².
[edit] Wakazi
Mwaka 2001 wakazi 3,669,349 walihesabiwa. Idadi kubwa ni Watswana na Kitswana ni lugha ya kwanza jimboni. Lugha ya pili ni Kiafrikaans.
Mji mkubwa ni Mafeking iliyounganishwa na Mmabatho (awali mji mkuu wa Bophuthatswana). Miji mingine yenye maana ni Potchefstroom, Klerksdorp, Brits, Rustenburg, Lichtenburg na Vryburg.
[edit] Uchumi
Migodi na uchimbaji madini huzalisha theluthi moja wa pato la jimbo. Zaidi ya 90% ya platini ya Afrika Kusini inapatikana karibu na Rustenburg na Brits. Pia robo ya dhahabu ya Afrika Kusini imepatikana jimboni.
Upande wa kilimo kuna hasa mahindi na mavuno yake ni theluthi ya mavuno ya taifa. Mazao mengine ni pamoja na alizeti, matunda, tumbako na pamba. Sehemu za magharibi na kaskazini zinafaa kwa ufugaji wa kondoo.