Lugha ya kidini

From Wikipedia

Lugha ya kidini ni lugha inayotumiwa pekee katika maisha ya kidini kama vile kwa shughuli za liturgia, sala au maandiko matakatifu wakati wasemaji au wasomaji wa luhja hii ya kidini hutumia lugha nyingine katika maisha ya kawaida.

Contents

[edit] Lugha za kale kama lugha za kidini

Mara nyingi lugha za kidini ni lugha za kale zinazohifadhiwa katika maisha ya kidini lakini katika maisha ya kawaida zimeshabadilika sana.

Mfano wake ni Kislavoni cha Kanisani kilichokuwa lugha ya kawaida ya makabila ya Kislavoni mnamo mwaka 800 BK wakati akina Methodio na Kyrilo wa Saloniki walipotafsiri vitabu vya kikristo kwa ajili ya misioni ya Waslanoni. Lakini lahaja mbalimbali za Kislavoni zimeendelea kubadilika na lugha mpya za kislavoni zimetokea kama vile Kirusi, Kibulgaria n.k.. Tangu karne nyingi hakuna mtu anatumia Kislavoni cha Kanisani kwa maisha ya kila siku lakini inaendelea kuwa lugha ya ibada na liturgia katika makanisa ya Kiorthodoksi ya mataifa ya Kislavoni kama vile vya Warusi, Wabulgaria, Waserbia.

Mfano mwingine ni Kisanskrit kilichokuwa lugha ya Waaria walioingia Uhindi takriban miaka 1,500 KK kikawa lugha ya maandiko matakatifu hufundishwa hadi leo lakini lugha za leo zimekuwa tofauti kabisa.

[edit] Lugha za kidini zisizotumiwa tena katika maisha ya kila siku

  • Kisanskrit katika Uhindu.
  • Kikopti katika Kanisa la Kikopti cha Misri
  • Ge'ez katika Kanisa la Orthodoksi la Ethiopia na Eritrea
  • Kislavoni cha Kanisani - taz. juu
  • Kilatini hutajwa mara nyingi kati ya lugha za kidini ya Kanisa Katoliki lakini kimehifadhiwa pia kama lugha ya elimu na utamaduni wa Ulaya nje ya matumizi ya kanisani.

[edit] Lugha za kidini zinazoendelea kuzungumzwa au zilizo karibu na lugha hai

Kuna pia lugha hai zinazotumiwa kama lugha za kidini nje ya eneo wanapokaa wasemaji wao. Mara nyingi hata katika lugha hizi za kidini maneno na matamshi yasiyo kawaida tena hutunzwa.

[edit] Kiarabu na Uislamu

Mfano wake mkuu ni Kiarabu kama lugha ya kidini kati ya Waislamu. Lugha ya Korani yenyewe haizungumzwi na Waarabu lakini inasikilizwa na kueleweka kwa Waarabu wengi. Sarufi yake bado ni ileile kama ya Kiarabu sanifu cha kisasa.

Lugha za Ulaya kama Kiingereza na Kijerumani zinatumia pia lugha ya pekee katika maisha ya kidini kutokana na tafsiri za Biblia zinazotunza maneno ya karne zilizopita zisizo kawaida tena katika maisha ya kila siku. Kwa Kiingereza ni hasa tafsiri ya Mfalme Yakobo (King James) na kwa Kijerumani ni tafsiri ya Martin Luther.

Tabia hizi zaonekana katika lugha na tamaduni nyingi.