Kidachi

From Wikipedia

Kidachi ni Kiswahili cha zamani kinachosikika hadi leo katika sehemu za Tanzania kwa ajili ya lugha ya Kijerumani au tabia za Wajerumani. Neno limetokana na neno "Deutsch" (tamka: doitsh) ambalo ni jinsi Wajerumani wenyewe wanajiita.

Kidachi, Mdachi/ Wadachi na Udachi zilikuwa Kiswahili cha kawaida kutokana na utawala wa Kijerumani katika Afrika ya Mashariki ya Kijerumani.

Tangu mwisho wa ukoloni wa Wajerumani mwaka 1918 na kuja kwa Waingereza wasemaji wa Kiswahili wamezoea zaidi kuwataja "Wadachi" kwa kutumia jina la asili ya Kiingereza yaani Kijerumani, Mjerumani / Wajerumani na Ujerumani.

Mara nyingi maneno yenye "-dachi" huchanganywa na neno la Kiingereza "Dutch" linalomaanisha Waholanzi.