1945
From Wikipedia
[edit] Matukio
- 8/9 Mei - Ujerumani inajisalimisha; mwisho wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia katika Ulaya.
- 26 Juni - Umoja wa Mataifa unaanzishwa mjini San Francisco na kuchukua nafasi ya Shirikisho la Mataifa.
- 16 Julai - Mlipuko wa kinyuklia wa kwanza karibu na Los Alamos (Marekani): Bomu la jaribio liitwalo „Trinity“ (Utatu) lenye nguvu ya kilotani 20 za TNT.
- 6 Agosti - Bomu la atomu la kwanza linatupwa na jeshi la anga la Marekani kwenye mji wa Hiroshima (Japani). Watu 70.000 wanakufa mara moja, jumla ya wafu kutokana na majeruhi na mnururisho itafikia idadi ya watu 240.000.
- 15 Agosti - Japani inajisalimisha; mwisho wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia katika Asia.
- 27 Disemba - Kuundwa kwa IMF (Shirika la Kimataifa la Fedha).
[edit] Waliozaliwa
bila tarehe
- Thomas Mapfumo, mwanamuziki kutoka Zimbabwe
[edit] Waliofariki
- 31 Machi - Hans Fischer (mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Kemia mwaka wa 1930)
- 9 Aprili - Dietrich Bonhoeffer
- 28 Aprili - Benito Mussolini (kiongozi wa Italia) anauawa na wanamgambo Waitalia wakomunisti.
- 30 Aprili - Adolf Hitler (kiongozi wa Ujerumani) anajiua mjini Berlin pamoja na mke wake Eva.
- 26 Septemba - Bela Bartok (mtungaji wa muziki Mhungaria)