Haile Selassie

From Wikipedia

Haile Selassie wa Ethiopia
Haile Selassie wa Ethiopia

Haile Selassie (23 Julai, 189227 Agosti, 1975) alikuwa mfalme wa Ethiopia. Alizaliwa katika kijiji kiitwacho Ejersa. Jina lake likiwa na maana ya Utatu Mtakatifu. Pia anafahamika kwa jina la Simba wa Yuda, Mfalme wa wafalme (H.I.M). Baba yake aliitwa Ras Makonnen, Gavana wa Harar, familia yake ina watoto 11. Alikuwa mkristo muumini wa dhehebu la orthodox.

Uzao wa mfalme Haile Selassie uliunganika na wa Menelik II ambao ni uzao wa Makeda malkia wa SHEBA ambao ni ukoo wa mfalme Solomon. Inaaminika kuwa sanduku la agano kwa mara ya mwisho lilikuwa Axum Ethiopia, kwa waumini wa imani ya Rastafari wanamwamini kama mtume wa Mungu aliyekuja kutimiza unabii ulioandikwa katika kitabu cha Zaburi, mlango 68:31 "Ethiopia itamnyoshea Bwana mikono yenye nguvu", na hii imetimilika baada ya kushinda nguvu uvamizi wa Waitalia chini ya Mussolini na kulifanya kuwa taifa la mfano dhidi ya uvamizi wa wakoloni.

Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Haile Selassie" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Haile Selassie kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.