Pasaka ya Kikristo
From Wikipedia
Mwaka | Ukristo wa Magharibi (Kalenda ya Gregori) |
Ukristo wa Mashariki (Kalenda ya Juliasi) |
---|---|---|
2000 | Aprili 23 | Aprili 30 |
2001 | Aprili 15 | |
2002 | Machi 31 | Mei 5 |
2003 | Aprili 20 | Aprili 27 |
2004 | Aprili 11 | |
2005 | Machi 27 | Mei 1 |
2006 | Aprili 16 | Aprili 23 |
2007 | Aprili 8 | |
2008 | Machi 23 | Aprili 27 |
2009 | Aprili 12 | Aprili 19 |
2010 | Aprili 4 | |
2011 | Aprili 24 | |
2012 | Aprili 8 | Aprili 15 |
2013 | Machi 31 | Mei 5 |
2014 | Aprili 20 | |
2015 | Aprili 5 | Aprili 12 |
2016 | Machi 27 | Mei 1 |
2017 | Aprili 16 | |
2018 | Aprili 1 | Aprili 8 |
2019 | Aprili 21 | Aprili 28 |
2020 | Aprili 12 | Aprili 19 |
Pasaka ya Kikristo ni sikukuu ya kukumbuka kufufuka kwake Yesu Kristo siku ya tatu baada ya kusulibiwa kwake. Inahesabiwa kuwa sikukuu muhimu kabisa katika Ukristo.
[edit] Jina la Pasaka
Jina la "Pasaka" limetokana na sherehe ya Pasaka ya Kiyahudi linaloitwa "פסח" (tamka: pasakh) kwa lugha ya Kiebrania. Kwa Kiswahili majina ya sherehe za Kikristo na Kiyahudi hazitofautiani. Asili yake ni ya kwamba kusulibiwa na kufufuka kwa Yesu Kristo kumetokea wakati wa sikukuu ya Pasaka ya Kiyahudi mnamo mwaka 30 BK. Wakristo wa kwanza ambao wote walikuwa Wayahudi walisheherekea sikukuu ya kiyahudi pamoja na kumbukumbu kwa ufufuo wa Yesu. Baadaye sherehe na pia tarehe zikawa tofauti.
[edit] Tarehe ya Pasaka
Tarehe ya Pasaka inafuata mwezi kwa hiyo sikukuu hiyo haina tarehe imara katika kalenda ya kawaida. Inapatikana katika Machi au Aprili. Mtaguso au Sinodi Kuu ya Nikea mwaka 325 BK iliamua ya kwamba Pasaka itasheherekewa Jumapili ya kwanza baada ya mwezi mpevu wa kwanza baada ya Machi 21 (tarehe ya sikusare machipuo ambayo ni siku ya usawa wa mchana na usiku hivyo mwanzo wa majira ya kuchipua katika kaskazini ya dunia). Kwa sababu mwezi mpevu baada ya Machi 21 inaweza kutokea kati ya Machi 22 na Aprili 19 tarehe ya Pasaka ambayo ni Jumapili inayofuata hutokea kati ya Machi 22 na Aprili 25.
Katika Ukristo kuna kalenda mbili zinazotumika hivyo pia tarehe mbili za Pasaka. Makanisa ya magharibi yaani Wakatoliki na Waprotestant hufuata Kalenda ya Gregori (ambayo imekuwa kalenda ya kawaida ya kimataifa), lakini Waorthodoksi wanaendelea kutumia kalenda iliyotangulia yaani Kalenda ya Juliasi.[[ Category:Kalenda]]