Kitawa

From Wikipedia

Kitawa ni aina ya chakula.

[edit] Utayarishaji

  • Maziwa ya mgando
  • Ndizi ng'ombe
  • Magadi

[edit] Utengenezaji

Ndizi humenywa na hukatwa katwa vijipande vidogo, hupikwa karibu na kuiva, huongezwa magadi vinapikwa vyote na kuiviana. Hupondwa pondwa na kuwa laini kama ugali. Baada ya hapo huwekwa maziwa ya mgando hukorogwa na kifaa kiitwacho kipekecho na kuwa laini kwa ajili ya matumizi.

[edit] Matumizi

Chakula hiki hupewa wanawake wakati wa uzazi, vijana wakati wa unyago, na wagonjwa. Chaweza kutumika kwa watu wa kawaida au watoto.