Ufilipino

From Wikipedia

Republika ng Pilipinas
Jamhuri ya Ufilipino
Flag of Ufilipino Nembo ya Ufilipino
Bendera Nembo
Wito la taifa: Maka-Diyos, Makatao, Makakalikasan, at Makabansa
("Kwa Mungu, watu, mazingira na nchi")
Wimbo wa taifa: Lupang Hinirang ("Nchi teule")
Lokeshen ya Ufilipino
Mji mkuu Manila
14°35′ N 121°0′ E
Mji mkubwa nchini Quezon City
Lugha rasmi Kifilipino na Kiingereza*
Serikali
Rais
Makamu wa Rais
Jamhuri
Gloria Macapagal Arroyo
Noli de Castro
Uhuru
Ilitangazwa
kujitawala
Ilitambuliwa
Katiba

12 Juni 1898
24 Machi 1934
4 Julai 1946
2 Februari 1987
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
300,000 km² (ya 72)
0.6
Idadi ya watu
 - 2006 kadirio
 - 2000 sensa
 - Msongamano wa watu
 
85,236,913[1] (ya 12)
76,504,077
276/km² (ya 42)
Fedha Philippine peso (piso) (PHP)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
PST (UTC+8)
(UTC)
Intaneti TLD .ph
Kodi ya simu +63
* Kicebuano, Kiilokano, Kihiligaynon, Kibikol, Kiwaray-waray, Likapampangan, Kipangasinan, Kinaray-a , Kimaranao , Kimaguindanao, Kitagalog, Kitausug ni lugha rasmi kieneo. Kihispania na Kiarabu hutambuliwa kwa msingi wa matumizi ya hiari.

Ufilipino Kifilipino : Pilipinas), ni nchi ya kisiwani kwenye Funguvisiwa ya Malay katika Asia ya Kusini-Mashariki. Mji mkuu ni Manila. Ina visiwa 7,107 vyenye eneo la 300,000 km².

Nchi iliitwa kwa jina la Kihispania "Las Islas Filipinas" (Visiwa vya Filipo) na Ruy López de Villalobos kwa heshima ya mfalme Filipo II wa Hispania. Hispania ilitwala eneo tangu 1565 hadi Mapinduzi ya Ufilipino wa 1896. Marekani ilitwaa visiwa 1898 katika vita ya Vita ya Marekani dhidi Hispania na kuvitawala kama koloni hadi Vita Kuu ya Pili ya Dunia wakati Ujaponi ikatwaa nchi kwa miaka minne.

Baada ya vita Ufilipino ikapewa uhuru wake.

Wakazi wengi wa Ufilipino hufuata Ukristo wa Kikatoliki (zaidi ya 80%) ambao ni urithi wa athira ya Kihispania. Lugha ya Kiingereza iliachwa na Marekani kama lugha rasmi pamoja na Kifilipino. Athira ya Kiislamu huonekana hasa kwenye kusini ya kisiwa cha Mindanao kwa jumla 5% za Wafilipino ni Waislamu wa dhehebu la Sunni.

Contents

[edit] Utawala

Kuna mikoa ifuatayo:

  • Ilocos (Region I)
  • Cagayan Valley (Region II)
  • Central Luzon (Region III)
  • CALABARZON (Region IV-A) ¹
  • MIMARO (Region IV-B) ¹
  • Bicol (Region V)
  • Visaya Magharibi (Region VI)
  • Visaya Kati (Region VII)
  • Visaya Mashariki (Region VIII)
  • Rasi ya Zamboanga (Region IX)
  • Mindanao Kaskazini (Region X)
  • Davao Region (Region XI)
  • SOCCSKSARGEN (Region XII) ¹
  • Caraga (Region XIII)
  • Mkoa wa Kujitawala wa Kiislamu wa Mindanao (ARMM)
  • Cordillera (CAR)
  • Mkoa wa Mji Mkuu Manila (Metro Manila)
Geography of the Philippines
Geography of the Philippines

[edit] Jiografia

Ufilipino ina visiwa 7,107 vinavyohesabiwa katika kundi tatu:

  • Luzon
  • Visaya
  • Mindanao.

Luzon ni kisiwa kikubwa na Mindanao ni kisiwa cha pili. Visaya ni kundi la visiwa katikati ya funguvisiwa. Mji mkuu wa Manila uko Luzon. Quezon City ni mji mkubwa. Cebu City ni mjimkubwa upande wa Visaya. Davao City ni mji mkuu wa Mindanao.

[edit] Viungo vya Nje

[edit] Tovuti rasmi

[edit] Mahali pengine

Nchi na maeneo ya Asia

Afghanistan | Armenia2 | Azerbaijan | Bahrain | Bangladesh | Bhutan | Brunei | China | Cyprus2 | Falme za Kiarabu | Georgia2 | Hong Kong3 | Indonesia | Iran | Iraq | Israel | Japan | Kambodia | Kazakhstan | Korea Kaskazini | Korea Kusini | Kuwait | Kirgizstan | Laos | Lebanon | Macau3 | Malaysia | Maldivi | Mongolia | Myanmar | Nepal | Oman | Pakistan | Palestina | Qatar | Urusi1 | Saudia | Singapore | Sri Lanka | Syria | Taiwan (Jamhuri ya China) | Tajikistan | Timor ya Mashariki | Ufilipino | Uthai | Uturuki1 | Turkmenistan | Uhindi | Uzbekistan | Vietnam | Yemen | Yordani

1. Nchi ina maeneo katika Asia na Ulaya. 2. Nchi hii iko Asia lakini kwa sababu za kihistoria au kiutamaduni inahesabiwa pia kati ya nchi za Ulaya. 3. Eneo la pekee la China.