Kasai
From Wikipedia
Mto wa Kasai | |
---|---|
|
|
Chanzo | Nyanda za juu za Bié (Angola) |
Mdomo | Kongo 170 km kaskazini ya Kinshasa |
Nchi | Angola na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo |
Urefu | 2,153 km |
Kimo cha chanzo | takriban 1,500 m |
Mkondo | hadi 12,000 m³/s |
Eneo la beseni | ?? km² |
Kasai ni tawimto mrefu wa Kongo unaoanza kwenye Nyanda za Juu za Bie za Angola. Chanzo iko kwa 12° kus/19° kask. kaskazini ya mji wa Luena. Inaelekea magahribi 400 km inapogeukia kaskazini. Sasa iko mpaka kati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Angola kwa 483 km. Katika sehemu hi kuna maporomoko makubwa kadhaa na lalio la mto unapanuka hadi 10 km.
Kabla ya kufikia Ilebo mto unageukia kuelekea magharibi-kaskazini. Sasa ni pia njia ya maji inayotumika na meli. Mto unapanuka kuwa bwawa la Wissmann. Karibu na mji wa Bandundu mto wa Kwango unajiunga na Kasai. Sehemu ya mwisho mto umejulikana kwa jina la Kwa hadi kufika Kongo.