Warshawa

From Wikipedia

Warshawa (Kipoland: Warszawa) ni mji mkuu wa Poland pia mji mkubwa mwenye wakazi milioni mbili.

Kitovu cha kihistoria cha Warshawa
Kitovu cha kihistoria cha Warshawa

Contents

[edit] Jiografia

Warshawa iko katikati ya nchi kando la mto Vistula (Kipoland:(polnisch Wisła) takriban 350 km kutoka Bahari Baltiki.

Warshawa ilivyoharibika baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia
Warshawa ilivyoharibika baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia

[edit] Historia

Warshawa imekuwa mji tangu karne ya 15 ikawa mji mkuu wa Poland mwaka 1596. Iliharibiwa mara nyingi katika historia yake hasa wakati wa vita kuu ya pili ya dunia. Wapoland walijaribu kuasi dhidi ya Wajerumani waloshika mji kati ya 1939 na 1944; pamoja na vofo vingi asilimia 90% za nyumba zote ziliharibiwa.

Baada ya vita mji ulijengwa upya mara nyingi kwa kurudisha nyumba zinazofanana na nyumba za kale.

[edit] Utamaduni

Kuna vyuo 66 pamoja na Chuo Kikuu cha Warshawa, vyuo vikuu vingine, nyumba za maigizo, opera na makumbusho mbalimbali.

[edit] Uchumi

Warshawa ni mji wa viwanda vingi vya kutengenezea chuma, mashine, motokaa na mengi mengine.


[edit] Picha za Warshawa

WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:


[edit] Viungo vya Nje

Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Warshawa" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Warshawa kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.