Yerusalemu

From Wikipedia

Yerusalemu

Ukuta wa Maombolezo na Kubba ya Mwamba mjini Yerusalemu

Seal

Flag
Jina la Kiebrania יְרוּשָׁלַיִם (Yerushalayim)
Jina la Kiarabu القـُدْس (al-quds);
rasmi: أورشليم القدس
(urshalim-al-quds)
Maana ya Jina Kiebrania: "Urithi wa amani",
Kiarabu: "patakatifu"
Utawala Mji
Wilaya
Wakazi 724,000 (2006)
Eneo 126,000  (126 km²)
Meya Uri Lupolianski
Tovuti rasmi www.jerusalem.muni.il

Yerusalemu (Kiebrania ירושלים yerushalayim, kar.: القدس al-quds) ni mji mwenye pande mbili katika Mashariki ya Kati. Kwa upande moja ni mji mkuu wa Israel. Kwa upande mwingine Yerusalemu ya mashariki inatazamiwa kuwa mji mkuu wa Palestina ingawa imetawaliwa na Israel pia tangu 1967. Israel imetangaza tangu 1980 Yerusalemu yote kuwa mji wake mkuu lakini nchi nyingi za dunia hazikubali azimio hili hivyo balozi za nchi za kigeni katika Israel ziko nje ya Yerusalemu.

Yerusalemu ina historia ndefu sana. Ni mji muhimu katika dini tatu za Uyahudi, Ukristo na Uislamu.

  • Ukuta wa Maombolezo ni patakatifu katika Uyahudi kwa sababu ni mabaki ya pekee ya Hekalu ya Yerusalemu ya zamani za Biblia.
  • Kanisa la Kaburi na Ufufuo wa Yesu kama mahali pa ufufuo wake pamoja na mahali pengi panapotajwa katika Agano Jipya ni patakatifu kwa Wakristo.
  • Msikiti wa Al-Aqsa pamoja na msikiti wa Kubba ya Mwamba ni mahali patakatifu kwa Waislamu kwa sababu zimetajwa katika Korani; Waislamu huamini ya kwamba hapa ni mahali pa miraji ya Mtume Muhammad.
Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Yerusalemu" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Yerusalemu kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.