Montevideo

From Wikipedia

Mji wa Montevideo.
Mji wa Montevideo.

Montevideo ni mji mkuu wa Uruguay na mji mkubwa nchini. Uko kwenye mdomo mpana wa mto Rio de la Plata. Karibu nusu ya watu wote wa Uruguay hukaa jijini; milioni 1.35 mjini penyewe na milioni 1.8 katika rundiko la jiji.

Jina la "Montevideo" lamaanisha "Naona mlima".

Wareno walijenga boma katika eneo la mji wa baadaya mnamo mwaka 1724. Walifukuzwa na Wahispania na tarehe 24 Desemba 1726 gavana Mhispania wa Bueno Aires Bruno Mauricio de Zabala aliunda mji wa Montevideo.

Tangu 1828 mji ulikuwa mji mkuu wa nchi ya Uruguay.

Mji ulikua kutokana na uhamiaji mkubwa kutoka Ulaya hasa Italia. Wakazi wengi wa Montevideo wana uzazi wa Kiitalia.


[edit] Viungo vya Nje