1492
From Wikipedia
[edit] Matukio
- 2 Januari - Mfalme Boabdil wa Granada anasalimisha mji wake kwa wafalme wa Hispania - mwisho wa utawala wa Kiislamu katika Hispania
- 30 Machi - Wafalme Ferdinand na Isabella wa Hispania waamuru kufukuzwa nchini kwa Wayahudi wote wasiopokea imani ya kikatoliki
- 31 Julai - Wahayudi wanafukuzwa Hispania
- Sultani Bayazid II wa Dola la Uturuki anatuma meli zake kwa shabaha ya kupokea Wayahudi wanaofukuzwa Hispania na kuwapeleka katika miji ya dola lake
- 2 Agosti - Kristoforo Kolumbus anaanza safari yake ya kwanza ya kuvuka Atlantiki akiamini ya kwamba anaelekea Uhindi
- 12 Oktoba - Kristoforo Kolumbus anafika kwenye visiwa vya Karibi akiamini ya kwamba amefika Uhindini.
- 28 Oktoba - Kristoforo Kolumbus anafika Kuba.
[edit] Waliozaliwa
[edit] Waliofariki