Bangkok

From Wikipedia

Hekalu ya Wat Phra Kaew mjini Bangkok
Hekalu ya Wat Phra Kaew mjini Bangkok
Bangkok ya kisasa
Bangkok ya kisasa

Bangkok ni mji mkuu na pia mji mkubwa wa Uthai katika Asia Kusini-Magharibi. Kuna wakazi milioni saba walioandikishwa lakini imekadiriwa ya kwamba jumla ya wakazi inafikia hadi milioni 14-15.

Mji uko kwa 13°45′N 100°31′E kando la mto Chao Phraya karibu na mdomo wake katika Ghuba la Uthai.

Mji ulianzishwa kama bandari kwa ajili ya mji mkuuwa kale Ayutthaya. Mfalme Rama I aliyeanzisha utawala wa familia ya kifalme ya Chakkri alijenga jumba lake hapo mtoni na kuanzisha mji mkuu mahala pa leo.

Kuna mahekalu 400 ya Ubuddha mjini hasa Wat Phra Kaew.

Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Bangkok" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Bangkok kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.