Ol Doinyo Lengai
From Wikipedia
Ol Doinyo Lengai (Kimaasai "mlima wa Mungu") ni mlima wa volkeno katika Tanzania ya Kaskazini. Iko takriban 120 km kaskazini-magharibi ya Arusha. Iko 25 km kusini ya Ziwa la Magadi (Tanzania - "Lake Natron").
Jina la mlima ni Kimaasai lamaanisha "mlima wa Mungu". Mlima una kimo cha 2690 m juu ya UB. Ni volkeno ya pekee duniani kutokana na aina ya lava yake inayotoka hali ya kiowevu (majimaji) lakini si moto sana (mnamo 500° - 600°C).
Ol Doinyo Lengai ilipuka tena katika Machi 2006.