Muammar al-Gaddafi
From Wikipedia
Amiri Muammar al-Gaddafi (Kiarabu:معمر القذافي Mu‘ammar al-Qadhāfī) ni kiongozi wa taifa la Libya.
Amezaliwa katika familia ya mabedawi (wafugaji wahamiaji) mnamo mwaka 1942. Baada ya masomo ya sheria kwenye chuo kikuu cha Libya alijiunga na jeshi 1963 akasoma kwenye chuo cha kijeshi cha Sandhurst (Uingereza) 1965.
1 Septemba 1969 pamoja na maafisa wenzake alipindua serikali ya mfalme Idris I na kutangaza Jamhuri ya Kiarabu ya Libya.
Ingawa hana cheo rasmi anaendelea kutawala nchi yake akiitwa "Kiongozi wa mapinduzi ya 1 Septemba ya Jamahiriya ya Ujamaa ya watu ya Kilibya-Kiarabu".