Papa
From Wikipedia
Papa ni cheo cha kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani. Cheo hiki kinaenda sambamba na askofu wa Roma.
Contents |
[edit] Asili ya cheo cha Papa
Kiasili neno la Kiitalia "papa" lamaanisha "Baba" likawa cheo kwa nia ya kumtaja askofu wa Roma kwa heshima ya pekee. Msingi wa heshima hii ni iamni ya kuwa askofu wa Roma ni mfuasi wa Petro mtume wa Yesu. Wakatoliki huamini ya kwamba Petro alipewa kazi ya Yesu ya kuongoza kanisa baada ya kifo chake na wajibu hii inaendelea kati ya wafuasi wa Petro kwenye kiti cha askofu wa Roma.
[edit] Majina ya mapapa
Papa tangu 2005 anaitwa Papa Benedikto XVI.
Papa huchaguliwa na makardinali wa kanisa katoliki baada ya kifo cha mtangulizi wake. Baada ya kuchaguliwa papa mpya anapata jina mpya. Papa Benedikto XVI aliitwa "Joseph Ratzinger".
[edit] Mkuu wa Vatikano
Papa ni pia mkuu wa nchi ya Mji wa Vatikano iliyopo ndani ya mji wa Roma (Italia).
[edit] Cheo cha Papa penginepo
Cheo cha Papa hutumiwa pia na mkuu wa Kanisa la Kikopti huko Misri. Cheo kinapatikana katika kanisa la Legio Mariae nchini Kenya.
![]() |
Makala hiyo kuhusu "Papa" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri". Ikiwepo makala kuhusu Papa kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili. |
Categories: Mbegu | Papa