Michael Jackson
From Wikipedia
Michael Jackson (alizaliwa 29 Agosti 1958) ni mwanamuziki mwenye asili ya kiafrika. Ana kipaji cha kuimba, kucheza na utunzi aina ya muziki wake ni Roki. Katika miaka ya 80 alivuma sana na albamu yake ya Thriller iliyovunja rekodi ya mauzo kwa kuuza nakala zaidi ya milioni 60 duniani kote. Michael Jackson alianza kuonekana jukwaani akiwa na miaka mitano tu. Ametokea familia ya wanamuziki ya Jackson Five. Hivi karibuni amekumbwa na kashfa za uzalilishaji wa watoto lakini hata hivyo mahakama yalimwona hana hatia.