Gorée

From Wikipedia

Ramani ya kale ya kisiwa(1772)
Ramani ya kale ya kisiwa(1772)
Gorée
Gorée
Gorée inavyoonekana kutoka baharini
Gorée inavyoonekana kutoka baharini
Gereza la watumwa
Gereza la watumwa
Kisiwa
Kisiwa

Gorée (kifaransa: Île de Gorée) ni kisiwa cha Atlantiki mbele ya pwani la Senegal na sehemu ya manisipaa ya Dakar. Ilijulikana kama kituo cha biashara ya watumwa. Hadi kukomeshwa kwa biashara hiyo mwaka 1848 watumwa walipelekwa kisiwani kutoka bara, kufungwa katika majela, kuuzwa kwenye minada na kubebwa Amerika kwa jahazi.

[edit] Jiografia

Kisiwa kina urefu wa 1000 m na upana wa 300m, eneo lake ni 36 ha.

[edit] Historia

Kisiwa kiliingia chini ya utawala wa Ureno mwaka 1444 BK. Uholanzi ilivamia Goree mwaka 1588. Katika karne zilizofuata Ufaransa na Uingereza zilishindana juu ya utawala wa kisiwa. Tangu 1815 kilikuwa chini ya Ufaransa. Mwaka 1879 idadi ya wakazi ilikuwa 2,956 (Wazungu 50, Chotara 750 na wengine Waafrika).

Makumbusho ya Gereza la Watumwa yamekuwa mahali pa utalii. Waamerika weusi walianza kufika kisiwani kutafuta nyayo za mamabu waliobebwa kutoka hapa kama watumwa wafungwa.

Tangu mwaka 178 Goree iliingizwa na UNESCO katika orodha la Urithi wa Dunia.

[edit] Viungo vya Nje

WikiMedia Commons