Bikini (atolli)
From Wikipedia
Bikini ni jina la atolli ya Mikronesia kwenye nchi ya Visiwa vya Marshall katika Pasifiki. Mahali pake ni 11°30'N 165°25'E. Ina visiwa vidogo 36 vinavyozungusha hori la ndani lenye urefu wa kilomita 4o na eneo la 594,2 km².
[edit] Makaburi ya manowari
Mwisho wa vita kuu ya pili ya dunia jeshi la Marekani lilizamisha manowari zilizoharibika na kutohitajiwa tena kwenye hori la ndani la atolli.
[edit] Milipuko ya kinyuklia
Kati ya 1946 na 1958 ilikuwa mahali pa majaribio ya kinyuklia ya Marekani. Zaidi ya mabomu 20 za kinyuklia zililipushwa hapa. Wakazi waliondolewa kabla ya majaribio na atolli ikawa kituo cha kijeshi. Waliporudi baada ya mwisho wa milipuko wengi aligonjeka kutokana na mnurulisho unaoendelea. Ilikuwa lazima kuwaondoa tena na sasa wanakaa kwneye kisiwa cha Kili au wengine katika mtaa wa vibanda kwenye atolli ya Majuro.
[edit] Bikini kama vazi la kuogelea la wanawake
Bikini imekuwa pia jina la vazi la kuogelea kwa wanawake lenye vipande viwili lililoanzishwa siku chache baada ya mlipuko wa kwanza mwaka 1946. Mwuzaji wa mavazi haya alitumia jina lililokuwa maarufu kama matangazo ya bure.