Afrika Kusini

From Wikipedia

+Republiek van Suid-Afrika (Kiafrikaans)
Republic of South Africa (Kiing.)
Riphabliki yeSewula Afrika (Kind.)
IRiphabliki yaseMzantsi Afrika
(Kixhosa)
IRiphabliki yaseNingizimu Afrika
(Kizulu.)
Rephaboliki ya Afrika-Borwa
(Kisotho kask.)
Rephaboliki ya Afrika Borwa
(Kisotho kus.)
Rephaboliki ya Aforika Borwa
(Kitswana)
IRiphabhulikhi yeNingizimu Afrika
(Sis.)
Riphabuliki ya Afurika Tshipembe
(Tsh.)
Riphabliki ra Afrika Dzonga
(Kitsonga)
Flag of South Africa Image:Za coa.gif
Bendera Coat of arms
Wito la taifa: /Xam: !ke e: ǀxarra ǁke
(English: "Unity In Diversity" or literally, "Diverse People Unite")
Wimbo wa taifa: National anthem of South Africa
Lokeshen ya South Africa
Mji mkuu Cape Town (Bunge)
Pretoria (Serikali)
Bloemfontein (Mahakama Kuu)
33°55′ S 18°25′ E
Mji mkubwa nchini Johannesburg
Lugha rasmi Kiafrikaans, Kiingereza, Kizulu, Kixhosa, Kiswati, Kindebele, Kisotho cha kusini, Kisotho cha Kaskazini, Kitsonga, Kitswana, Kivenda
Serikali Jamhuri
Thabo Mbeki
Uhuru
Maungano ya Afrika Kusini
31 Mei 1910
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
1,221,037 km² (ya 25)
kidogo sana
Idadi ya watu
 - Julai 2005 kadirio
 - 2001 sensa
 - Msongamano wa watu
 
47,432,000 [1] (ya 26)
44,819,278
39/km² (ya 136)
Fedha Rand (ZAR)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
(UTC+2)
not observed (UTC+2)
Intaneti TLD .za
Kodi ya simu +27
1.) angalia: Makadirio ya idadi ya watu ni pamoja na vifo kutokana na UKIMWI.

Afrika Kusini ni nchi kubwa ya Afrika ya Kusini yenye wakazi takriban milioni 45. Imepakana na Namibia, Botswana, Zimbabwe, Msumbiji na Uswazi. Nchi ya Lesotho iko ndani ya eneo la Afrika Kusini.

Mji mkubwa ni Johannesburg. Wajibu wa mji mkuu yamegawiwa kwa mji mitatu: Cape Town ni makao ya Bunge, Pretoria ni makao ya Serikali na Bloemfontein ni makao ya Mahakama Kuu.

Nchi ina majina rasmi 11 kutokana na lugha rasmi 11. Ndizo Kiafrikaans, Kiingereza, Kizulu, Kixhosa, Kiswati, Kindebele, Kisotho cha kusini, Kisotho cha Kaskazini, Kitsonga, Kitswana, Kivenda.

Kati ya watu mashuhuri sana wa Afrika Kusini ni Nelson Mandela aliyekuwa rais kati ya 1994 hadi 1999. Wengine ni Christian Barnaard (daktari wa kwanza duniani aliyetumia moyo wa mtu kwa mtu mwingine) na Shaka Zulu aliyekuwa kiongozi wa kijeshi kabla ya ukoloni.

ramani ya Afrika Kusini
ramani ya Afrika Kusini

Contents

[edit] Uchumi

Kiuchumi Afrika Kusini ni nchi yenye pande mbili kabisa. Sehemu ya uchumi ina hali ya kimaendeleo kabisa ikiwa viwanda na huduma za Afrika Kusini zinalingana na hali ya juu kabisa duniani na hali ya maisha ya wananchi waliomo katika sekta hii inalingana na nchi kama Australia au Ulaya ya magharibi. Kwa upande mwingine hali ya maisha ya sehemu kubwa ya wananchi ni umaskini kama katika sehemu nyingine za Afrika au Uhindi wa mashambani. Lakini kwa ujumla hali ya maisha iko juu kuliko nchi nyingi za Afrika.

Sekta muhimu za uchumi ni migodi ya kuchimba dhahabu au almasi, viwanda na huduma kama benki au bima.


[edit] Utawala na muundo wa shirikisho

Afrika Kusini ni shirikisho. Katiba mpya ya 1997 iliendeleza muundo huu uliundwa kama "Umoja wa Afrika Kusini" baada ya vita ya makaburu dhidi Uingereza. Afria ya Kusini ya kale ilikuwa na majimbo manne ya (Rasi, Natal, Dola Huru la Mto Orange na Transvaal). Maeneno makubwa yaliyokaliwa na Waafrika yalibaki nje katika katiba ya Apartheid yakiitwa bantustan (au: homeland). Katiba mpya ilichora mipaka upya.

[edit] Majimbo ya Afrika Kusini

Ramani ya majimbo na wilaya za Afrika Kusini
Ramani ya majimbo na wilaya za Afrika Kusini

Mji mkuu wa jimbo watajwa katika mabano.

  1. Rasi ya Magharibi (Western Cape)¹ (Cape Town) kifupi: WC
  2. Rasi ya Kaskazini (Northern Cape) (Kimberley) kifupi: NC
  3. Rasi ya Mashariki (Eastern Cape) (Bhisho) kifupi: EC
  4. KwaZulu-Natal (Pietermaritzburg²) kifupi: KZ, KZN or KN
  5. Dola Huru (Free State) (Bloemfontein) kifupi: FS
  6. Kaskazini-Magharibi (Mafikeng) kifupi: NW
  7. Gauteng (Johannesburg) kifupi: GT or GP
  8. Mpumalanga (Nelspruit) kifupi: MP
  9. Limpopo (Polokwane) kifupi: LP

[edit] Miji Mikubwa

Hii ni miji/ manisipaa/ jiji kumi yenye wakazi wengi nchini.

Na. Munisipaa au Jiji Wakazi (2001) Wakazi (1996) Asilimia ya badiliko
1996-2001
1. Johannesburg, Gauteng 3,225,812 2,639,110 22.2%
2. Durban, KwaZulu-Natal 3,090,117 2,751,193 12.3%
3. Cape Town, Rasi ya Magharibi 2,893,251 2,563,612 12.9%
4. East Rand, Gauteng 2,480,282 2,026,807 22.4%
5. Pretoria, Gauteng 1,985,984 1,682,701 18.0%
6. Port Elizabeth, Rasi ya Mashariki 1,005,776 969,771 3.7%
7. East London, Rasi ya Mashariki 701,881 682,287 2.9%
8. Vereeniging, Gauteng 658,422 597,948 10.1%
9. Bloemfontein, Dola Huru 645,441 603,704 6.9%
10. Thohoyandou, Limpopo 584,469 537,454 8.7%

List of largest cities in South Africa by population

[edit] Jeshi

Jeshi la Afrika Kusini ina silaha za kisasa kushinda nchi zote za majirani. Uchumi unawezesha nchi ya kutumia kiasi kikubwa kwa ajili ya jeshi kuliko nchi zote za Afrika kusini ya Sahara.

Afrika Kusini iliwahi kuwa na silaha za kinyuklia lakini ilizibomoa baada ya mwaka 1993.

[edit] Viungo vya nje

Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Afrika Kusini" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Afrika Kusini kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.


Nchi za Afrika Bara la Afrika
Afrika ya Kati (Jamhuri ya) | Afrika Kusini | Algeria | Angola | Benin | Botswana | Burkina Faso | Burundi | Cabo Verde | Chad |Cote d'Ivoire | Djibouti | Eritrea | Gabon | Gambia | Ghana | Guinea | Guinea Bisau | Guinea ya Ikweta | Kamerun | Kenya | Komori | Kongo (Jamhuri ya) | Kongo (Jamhuri ya Kidemokrasia ya) | Lesoto | Liberia | Libya | Madagaska | Malawi | Mali | Misri | Morisi (Visiwa vya) | Mauritania | Moroko | Msumbiji | Namibia | Niger | Nigeria | Rwanda | Sahara ya Magharibi | Sao Tome na Principe | Senegal | Shelisheli | Sierra Leone | Somalia | Sudan | Tanzania | Togo | Tunisia | Uganda | Uhabeshi | Uswazi | Zambia | Zimbabwe
Maeneo ya kiafrika ambayo ni sehemu za nchi nje ya Afrika
Ufaransa: Mayotte · Réunion | Hispania: Visiwa vya Kanari · Ceuta · Melilla | Ureno: Visiwa vya Madeira | Uingereza: · Kisiwa cha St. Helena · Kisiwa cha Diego Garcia