Rudolf Christoph Eucken
From Wikipedia
Rudolf Christoph Eucken (5 Januari, 1846 – 14 Septemba, 1926) alikuwa mwanafalsafa na mwandishi kutoka nchi ya Ujerumani. Alitafsiri vitabu vya Aristoteli na kuandika vitabu kuhusu maadili na dini. Mwaka wa 1908 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fasihi.