Transkei
From Wikipedia

Transkei ilikuwa Bantustan ya kwanza ya Afrika Kusini iliyotangazwa kuwa nchi ya pekee. Eneo lake lilikuwa 43,800 km² na idadi ya wakazi takriban milioni 3.2. mji mkuu ilikuwa Umtata (au Mthatha).
Neno Transkei lamaanisha "ng'ambo ya mto Kei". Pamoja na Bantustan nyingine ca Ciskei ("upande huu wa mto Kei") ilipangwa kuwa bantustan kwa ajili ya Waxhosa. Transkei ilikuwa na takriban nusu ya Waxhosa wote ingawa hali halisi wengi walikaa na kufanya kazi Afrika Kusini ingawa bila haki za wananchi.
Transkei ilipewa madaraka ya kujitawala 1963 ikatangazwa kuwa nchi huria 26 Oktoba 1976 lakini hakuna nchi iliyotambua Ciskei kama nchi ya pekee.
Rais wa Transkei alikuwa chifu Kaizer Daliwonga Matanzima hadi 1987 alipopinduliwa na mkuu wa jeshi lake Bantu Holomisa. Kaizer Mantanzima alikuwa mpwa wake Nelson Mandela lakini hakukubali na siasa ya ANC. Akajaribu kwa muda kuwa na siasa mbali na Afrika Kusini lakini alishindwa kwa sababu serikali yake ilitegemea ruzuku kutoka serikali ya Pretoria.
Wakati wa mwisho wa apartheid mwaka 1994 Transkei iliunganishwa tena na Afrika Kusini mpya.