Asha-Rose Mtengeti Migiro

From Wikipedia

Asha-Rose Migiro na Katibu Mkuu Ban Ki-moon
Asha-Rose Migiro na Katibu Mkuu Ban Ki-moon

Asha-Rose Mtengeti Migiro (*1956) ni Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa. Amepewa cheo hiki na Katibu Mkuu Ban Ki-moon tar. 5 Januari 2007.

Hadi kuteuliwa kwa cheo cha UM alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Tanzania tangu Januari 2006. Wajibu huo alipewa na rais Jakaya Kikwete aliyemteua kumfuata katika wizara ya mambo ya nje iliyoshikwa awali na Kikwete mwenyewe.

Chini ya raisi Benjamin Mkapa Migiro alikuwa Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto. Alikuwa mbunge kwa njia ya kiti maalumu cha wanawake.

Kabla ya kujiunga na siasa alifundisha kwenye Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Alisoma digrii za bachelor na master Dar es Salaam. Mwaka 1992 akaongeza cheti cha udaktari wa sharia kwenye Chuo kikuu cha Konstanz (Ujerumani). Akarudi Tanzania alipoanza kufundisha. Akawa mwanachama wa CCM

Akiwa Mwislamu ameolewa na Cleophas Migiro wana watoto wawili wa kike.

[edit] Viungo vya Nje

Habari za Asha-Rose Mtigiro kwenye tovuti rasmi ya Bunge la Tanzania

Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Asha-Rose Mtengeti Migiro" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Asha-Rose Mtengeti Migiro kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.

Lugha nyingine