Usultani wa Zanzibar

From Wikipedia

Eneo la Usultani wa Zanzibar mnamo 1885
Eneo la Usultani wa Zanzibar mnamo 1885

Usultani wa Zanzibar ilikuwa nchi kwenye pwani la mashariki ya Afrika kati ya 1856 na 1964. Tangu 1890 ilikuwa nchi lindwa chini ya Uingereza.

Contents

[edit] Sayyi Said kuhamia Unguja

Usultani ulianzishwa wakati Sultani Sayyid Said alipoamua kuhamisha makao makuu yake kutoka Maskat (Omani) kwenda Unguja. Sayyid Said alikuwa Sultani wa Omani tangu 1804. Aliimarisha utawala wa Omani juu ya pwani la Afrika ya Mashariki. Mwaka 1829 alifaulu kuteka Mombasa iliyokuwa mji wa pekee wa kujitegemea kati ya miji yote ya Uswahilini.

Visiwa vya Unguja na Pemba vilikuwa chini ya Omani tangu 1689 Wareno walipofukuzwa katika pwani za Uswahilini.

[edit] Biashara ya karafuu na watumwa

Sayyid Said aliona nafasi kubwa ya biashara ya karafuu kwa ajili ya soko ya Uhindi na penginepo. 1829 akaanzisha mashamba ya mikarafuu kwa kutumia kazi ya watumwa kutoka bara. Biashara ikabadilisha uso wa mji wa Zanzibar ya karne ya 19 iliyowahi kuwa kijiji kikubwa tu ya vibanda kando la boma lililojengwa na Omani kama kizuizi dhidi ya Wareno.

Baada ya azimio la mwaka 1832 la kuhamisha mji mkuu wa Omani kwenda Unguja idadi ya wakazi wa mji ulikua haraka. Nchi za nje zikatambua mji mkuu mpya na kujenga uhusiano. Ubalozi wa Marekani ulijengwa 1837, Uingereza ukafuata 1841 na Ufaransa 1844. Sultani mwenyewe aliondoka Maskat kabisa mwaka 1840. Kukua kwa Zanzibar kulisababisha kukonda kwa mji wa Maskat

Bendera ya Usultani wa Zanzibar
Bendera ya Usultani wa Zanzibar

[edit] Kugawiwa kwa Omani ilikuwa mwanzo wa Zanzibar

Baada ya kifo cha Sayyid Sultan mwaka 1856 usultani wa Oman uligawiwa kati ya wanawe. Sayyid Majid bin Said Al-Busaid (1834/5–1870) akawa Sultani wa kwanza wa Zanzibar na kakaye Sayyid Thuwaini bin Said al-Said akawa Sultani wa Oman akitawala nchi bila maeneo ya Afrika ya Mashariki.

Usultani mpya ulikuwa nchi yenye nguvu kati ya Rasi Delgado (mpakanani na koloni ya Kireno ya Msumbiji) hadi Mogadishu. Athira yake ilienea kupitia njia za misafara ya pembe za ndovu na watumwa hadi mto Kongo. Wafanyabiashara kama Tippu Tip waliokuwa raia wa Usultani wakapita Tabora na Ujiji kwenda ziwa Tanganyika na kuingia ndani ya Kongo. Wapagazi wao walibeba bidhaa kutoka Zanzibar zilizobadilishwa kwa pembe za ndovu hasa. Watumwa walikamatwa au kununuliwa wakabeba pembe hadi pwani.

Jumba la Sultani Zanzibar
Jumba la Sultani Zanzibar

[edit] Sayyid Bargash

Sultani wa pili wa Zanzibar penyewe Sayyid Bargash alijitahidi kujenga uhusiano na nchi za nje. Alifunga soko la watumwa Zanzibar mjini kulingana na mapatano ya mimataifa lakini akavumilia biashara ya watumwa kuendelea chinichini. Wakati wa Bargash majengo mengi ya Mji Mkongwe yakajengwa.

Mwishowe wa utawala wake aliona kupungukiwa wa eneo lake kutokana na mashindano ya nchi za Ulaya ya kuenea katika Afrika baada ya mkutano wa Berlin. 1885 Karl Peters alifanya mikataba ya ulinzi na watawala wadogo barani ya Tanganyika waliokuwa chini ya Sultani. Upingamizi wa Sultani ulishindikana kwa sababu Wajerumani walituma manowari Unguja akapaswa kukubali maeneneo mapya ya Wajerumani.

[edit] Kuenea kwa ukoloni

1886 mkataba kati ya Uingereza na Ujerumani ulibana eneo la sultani barani katika kanda yenye upana wa maili kumi kati ya Rasi Delgado na Mogadishu. Bargash na mfuasi wake Khalifa bin Said waliamua kuuza maeneo haya au kuyakodisha.

  • 1887/8 pwani la Kenya ikakodishwa kwa Waingereza. Wakati wa uhuru wa Kenya sehemu hii ikaingizwa katika Jamhuri ya Kenya.
  • Pwani la Tanganyika ikakodishwa kwa Wajerumani mwaka 1888 na kuuzwa mwaka 1890.
  • Miji kwenye pwani la Somalia ikakodishwa kwa Italia mwaka 1892 ikauzwa 1906, Mogadishu 1924.

Hali halisi usultani ukabaki na visiwa viwili vya Unguja na Pemba tu.

Waingereza walikuwa walisita kuhusu Zanzibar lakini baada ya jaribio la Karl Peters la kufanya mkataba wa Sultani na kuingiza visiwa katika Afrika ya Mashariki ya Kijerumani Uingereza uliamua kutafuta utawala wa visiwa.

[edit] Mkataba wa Zanzibar-Heligoland na mwisho wa uhuru

Mkataba wa Zanzibar-Helgoland kati ya Ujerumani na Uingereza ulileta patano la kuwa Zanzibar itakuwa chini ya Uingereza. Tangu 1890 waziri mkuu wa Sultani alikuwa Mwingereza aliyeopkea amri zake kutoka London. Tangu 1913 nafasi ilichukuliwa na afisa mkazi mkuu.

[edit] Uhuru 1963 na mapinduzi

Zanzibar ilipata uhuru wake 10 Desemba 1963. Uhuru wa usultani ukadumu muda kidogo tu. Mapinduzi ya 12 Januari 1964 yakampindua Sultani. Mauaji ya familia nyingi zenye asili ya kiarabu yakafuata. 26 Aprili 1964 Zanzibar ikaunganika na Tanganyika kuwa Jamhuru ya Maungano ya Tanzania.

[edit] Masultani wa Zanzibar

  1. Sayyid Said (1856–1870)
  2. Barghash bin Said (1870–1888)
  3. Khalifah bin Said (1888–1890)
  4. Ali bin Said (1890–1893)
  5. Hamad bin Thuwaini (1893–1896)
  6. Khalid bin Barghash (1896)
  7. Hamud bin Muhammed (1896–1902)
  8. Ali bin Hamud (1902–1911) (abdicated)
  9. Khalifa bin Harub (1911–1960)
  10. Abdullah bin Khalifa (1960–1963)
  11. Jamshid bin Abdullah (1963–1964)

[edit] Mawaziri

  1. Sir Lloyd William Matthews, (1890 hadi 1901)
  2. A.S. Rogers, (1901 hadi 1906)
  3. Arthue Raikes, (1906 hadi 1908)
  4. Francis Barton, (1906 hadi 1913)

[edit] Maafisa wakazi wakuu

  1. Francis Pearce, (1913 hadi 1922)
  2. John Sinclair, (1922 hadi 1923)
  3. Alfred Hollis, (1923 hadi 1929)
  4. Richard Rankine, (1929 hadi 1937)
  5. John Hall, (1937 hadi 1940)
  6. Henry Pilling, (1940 hadi 1946)
  7. Vincent Glenday, 1946 hadi 1951)
  8. John Sinclair, (1952 hadi 1954)
  9. Henry Potter, (1954 hadi 1959)
  10. Arthur Mooring, (1959 hadi 1963)