Polynesia ya Kifaransa
From Wikipedia
|
|||||
Wito la taifa: "Tahiti Nui Mare'are'a" "Tahiti kubwa katika mvuke wa dhahabu" |
|||||
Wimbo wa taifa: La Marseillaise | |||||
Mji mkuu | Papeete |
||||
Mji mkubwa nchini | Papetee | ||||
Lugha rasmi | Kifaransa | ||||
Serikali | Eneo la ng'ambo la Ufaransa Jacques Chirac Gaston Tong Sang |
||||
Eneo la ng'ambo la Ufaransa Sikukuu ya Mapinduzi ya Ufaransa |
14 Julai (1789) | ||||
Eneo - Jumla - Maji (%) |
4,167 km² (ya 173) 12 |
||||
Idadi ya watu - Julai 2006 kadirio - 2002 sensa - Msongamano wa watu |
260,338 (ya 181) 245,405 64/km² (ya 130) |
||||
Fedha | CFP franc (XPF ) |
||||
Saa za eneo - Kiangazi (DST) |
(UTC-10) (UTC) |
||||
Intaneti TLD | .pf | ||||
Kodi ya simu | +689 |
Polynesia ya Kifaransa (Kifaransa: Polynésie française, Kitahiti: Pōrīnetia Farāni) ni eneo la ng'ambo la Ufaransa katika Pasifiki ya kusini. Eneo lake ni funguvisiwa mbalimbali za Polynesia. Inayojulikana zaidi ni Tahiti pamoja na mji mkuu wake wa Papeete ambayo ni pia mji mkuu wa eneo lote.
[edit] Jiografia
Visiwa, funguvisiwa na atolli za Polynesia ya Kifaransa vina eneo la 4,167 km² jumla vilivyosambazwa katika kilomita za mraba 2,500,000 za bahari.
Visiwa vyote vimegawiwa katika tarafa tano ambazo ni vikundi vya visiwa vyenye funguvisiwa ndani yao ni kama zifuatazo
- Visiwa vya Marquesas katika kaskazini karibu zaidi na Hawaii penye kundi mbili za visiwa vya kaskazini na ya kusini
- Visiwa vya Tuamoto-Gambier ni eneo kubwa la Polynesia ya Kifaransa lenye funguvisiwa mbili za Tuamoto (atolli 76) na Gambier (visiwa 26)
- Visiwa vya Shirikia (Visiwa vya Society) 13 vya asili ya kivoleno ambavyo ni sehemu penye wakazi wengi vimegawiwa kwa tarafa mbili za
- tarafa ya Visiwa upande wa upepo pamoja na kisiwa ikuu cha Tahiti chenye nusu ya wakazi wote wa Polynesia ya Kifaransa
- tarafa ya Visiwa mbali na upepo
- Visiwa vya Austral (Visiwa vya Kusini) vyenye funguvisiwa viwili Tubuaï na Bass.