Teinainano
From Wikipedia
Teinainano (au: South Tarawa) ni mji mkuu wa nchi ya visiwani ya Kiribati katika Pasifiki.
Manisipaa ya Teinainano (Teinainano Urban Council - TUC) yenye wakazi 36,717 inajumlisha vijiji na miji midogo ya kisiwa kirefu kwenye kusini ya atolli ya Tarawa. Anwani ya kijiografia ni 1°19'N 172°58'E.
Majengo ya serikali yapo hasa mjini Bairiki ambao ni kisiwa kidogo kilichounganishwa na sehemu nyingine za Teinainano kwa madaraja.
Kuna Chuo cha Ualimu cha Kiribati pamoja na tawi la Chuo Kikuu cha Pasifiki ya Kusini. Kuna pia ofisi kuu za makanaisa makubwa.