Indonesia

From Wikipedia

Republik Indonesia
Republic of Indonesia
Flag of Indonesia Coat of arms ya Indonesia
Bendera Coat of arms
Wito la taifa: Bhinneka Tunggal Ika
(Kijava/Kikawi: Umoja katika tofauti)
Itikadi: Pancasila
Wimbo wa taifa: Indonesia Raya
Lokeshen ya Indonesia
Mji mkuu Jakarta
6°08′ S 106°45′ E
Mji mkubwa nchini Jakarta
Lugha rasmi Indonesian
Serikali
Rais
Makamu Rais
Jamhuri
Susilo Bambang Yudhoyono
Jusuf Kalla
Uhuru
Kutangaza
Kutambuliwa
Kutoka Uholanzi
17 Agosti 1945
27 Desemba 1949
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
1,904,569 km² (16th)
4.85%
Idadi ya watu
 - 2005 kadirio
 - 2000 sensa
 - Msongamano wa watu
 
222,781,000 (4th)
206,264,595
116/km² (84th)
Fedha Rupiah (IDR)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
various (UTC+7 to +9)
not observed (UTC+7 to +9)
Intaneti TLD .id
Kodi ya simu +62

Indonesia ni nchi ya visiwa katika Asia ya Kusini-Mashariki. Iko upande wa Kusini-Mashariki kati ya Bahari ya Uhindi na Pasifiki. Ni sehemu ya funguvisiwa ya Malay.

Indonesia imepakana na Papua Guinea Mpya kwenye kisiwa cha Guinea Mpya pia na Timor ya Mashariki kwenye kisiwa cha Timor halafu na Malaysia kwenye kisiwa cha Borneo. Nchi zilizo karibu ni Australia, Singapore na Ufilipino.

[edit] Jiografia

Indonesia ni nchi ya visiwa 18,000 ilhali zaidi ya 6,000 kati ya hivi vinakaliwa na watu. Visiwa vikubwa vyenye wakazi wengi ni hasa vitano:

  • Java
  • Sumatra
  • Kalimantan (Borneo ya Kiindonesia)
  • Guinea Mpya (pamoja na nchi ya Papua Guinea Mpya)
  • Sulawesi.

[edit] Wakazi, lugha, utamaduni

Nchi ina wakazi 238,452,952 (2004) hivyo ina nafasi ya nne kati ya mataifa makubwa duniani. Ni nchi penye Waislamu wengi duniani.

Lugha rasmi ni Bahasa Indonesia (Kiindonesia) iliyoundwa katika karne ya 20 kama lugha ya kitaifa kutokana na lahaja ya Kimalay.

Idadi kubwa ya wakazi (86 %) wanahesabiwa kuwa Waislamu, 11 % kama Wakristo, 2 % Wahindu na 1 % Wabuddha. Wahindu wako hasa kwenye kisiwa cha Bali.

[edit] Historia

Visiwa vya Indonesia viliathiriwa na utamaduni wa Uhindi. Kisiasa palikwa na falme nyingi. Tangu karne ya 17 Waholanzi walianza kujenga vituo na kueneza utawala wao. Waliita koloni yao "Uhindi wa Kiholanzi" ("Nederlands-Indië").

Wakati wa vita kuu ya pili ya dunia Japani ikatwaa visiwa na kuwafukuza Waholanzi. Mwisho wa vita kiongozi Sukarno akatangaza Indonesia kama nchi huru. Waholanzi walijaribu kuruisha utawala wao lakini walilazimishwa na Marekani kukubali uhuru wa nchi.

Nchi na maeneo ya Asia

Afghanistan | Armenia2 | Azerbaijan | Bahrain | Bangladesh | Bhutan | Brunei | China | Cyprus2 | Falme za Kiarabu | Georgia2 | Hong Kong3 | Indonesia | Iran | Iraq | Israel | Japan | Kambodia | Kazakhstan | Korea Kaskazini | Korea Kusini | Kuwait | Kirgizstan | Laos | Lebanon | Macau3 | Malaysia | Maldivi | Mongolia | Myanmar | Nepal | Oman | Pakistan | Palestina | Qatar | Urusi1 | Saudia | Singapore | Sri Lanka | Syria | Taiwan (Jamhuri ya China) | Tajikistan | Timor ya Mashariki | Ufilipino | Uthai | Uturuki1 | Turkmenistan | Uhindi | Uzbekistan | Vietnam | Yemen | Yordani

1. Nchi ina maeneo katika Asia na Ulaya. 2. Nchi hii iko Asia lakini kwa sababu za kihistoria au kiutamaduni inahesabiwa pia kati ya nchi za Ulaya. 3. Eneo la pekee la China.
Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Indonesia" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Indonesia kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.