Visiwa vya Marshall

From Wikipedia

Aolepān Aorōkin M̧ajeļ
Republic of the Marshall Islands
Jamhuri ya Visiwa vya Marshall
Flag of Marshall Islands Nembo ya Marshall Islands
Bendera Nembo
Wito la taifa: "Jepilpilin ke ejukaan"
Wimbo wa taifa: Forever Marshall Islands
Lokeshen ya Marshall Islands
Mji mkuu Majuro
7°7′ N 171°4′ E
Mji mkubwa nchini Majuro
Lugha rasmi Marshallese, Kiingereza
Serikali
Rais

Kessai Note
Uhuru
kutoka Marekani

21 Oktoba 1986
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
181 km² (ya 213)
‘‘(kidogo sana)’’
Idadi ya watu
 - Julai 2005 kadirio
 - 2003 sensa
 - Msongamano wa watu
 
61,963 (ya 205)
56,429
326/km² (ya 28)
Fedha US Dollar (USD)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
(UTC+12)
(UTC)
Intaneti TLD .mh
Kodi ya simu +692

Visiwa vya Marshall ni nchi ya visiwani ya Mikronesia katika Pasifiki ya magharibi. Nchi jirani katika bahari ni Nauru, Kiribati, Shirikisho la Mikronesia na eneo la Marekani la Kisiwa cha Wake. Atolli ya Majuro ina nafasi ya mji mkuu.

[edit] Jiografia

Eneo la visiwa vya Marshall ni safu mbili za visiwa au atolli zinazoelea sambamba:

  • safu ya Ratak upande wa mashariki na
  • safu ya Ralik upande wa magharibi.

Kwa jumla kuna visiwa na vipande vya atolli 1,150 katika eneo la bahari la 1,900,000 km².

[edit] Historia

Jina limetokana na nahodha Mwingereza John Marshall aliyetembelea eneo hili mwaka 1788 na kulichora katika ramani. Hata hivyo visiwa vilikaliwa tayari tangu karne nyingi na watu kutoka Mikronesia lakini jina la kizungu limebaki kwa ajili ya jumla ya visiwa. Mwisho wa karne ya 19 Ujerumani ulianzisha ukoloni juu ya visiwa ukaviunganisha kiutawala na Guinea Mpya yya Kijerumani. Katika vita kuu ya kwanza ya dunia vilitwaliwa na Japani iliyoendelea kutawala visiwa kama eneo lindwa kwa niaba ya shirikisho la mataifa. Baada ya vita kuu ya pili ya dunia vilikuwa eneo chini ya Marekani.

1979 visiwa vimepata madaraka ya kujitawala na kupokea uhuru kufuatana na azimio la Umoja wa Mataifa 1990.

[edit] Majaribio ya kinyuklia

Kuanzia 1946 Marekani ilitumia visiwa kwa ajili ya majaribio ya mabomu ya nyuklia. Hadi 1958 ilitokea milipuko 6,913 kwenye atolli za Bikini na Eniwetok. Hadi leo kuna wakazi wa visiwa wanavyoteswa na maradhi yaliyosababishwa na mnurulisho wa mabomu haya. Bikini haitawezekana kukaliwa na watu kabla ya mwaka 2050, Eniwetok haifai kwa makazi ya kibinadamu kwa miaka 24,000 inayokuja.


Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Visiwa vya Marshall" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Visiwa vya Marshall kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.