Ganda la dunia

From Wikipedia

Ganda la dunia ni tabaka ya juu ya sayari yetu. Ni sehemu ya tabakamwamba.

Ganda ni jumla la mabamba yanayosukumwa na nguvu ya shindikizo kutoka kitovu cha dunia.

Mwamba wa ganda hutokea pale ambako magma (yaani mwamba moto wa kiowevu) inapanda juu kwenye migongo iliyoko katikati ya msingi wa bahari inapopoa na kuganda.

Kinyume chake sehemu za ganda la dunia huzama chini pale ambako bamba moja linajisukuma chini ya bamba lingine na kuyeyuka katika magma ya koti ya dunia.

Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Ganda la dunia" inatumia neno ambalo si kawaida na matumizi yake ni jaribio kwa jambo linalotajwa.
Wasomaji wanaombwa kuchangia mawazo yao.

Kamusi za Kiswahili ama zinatofautiana kuhusu matumizi ya neno hili au hazieleweki au hazina neno kwa jambo linalojadiliwa.

Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Ganda la dunia" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Ganda la dunia kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.