Everest (mlima)

From Wikipedia

Mlima Everest
Mlima Everest

Mlima Everest ni mlima mkubwa duniani mwenye kimo cha 8,848 m juu ya UB. Ni sehemu ya safu ya milima ya Himalaya.

Kilele chake kipo mpakana wa Nepal na China (Tibet).

Watu wa kwanza wa kufika kwenye kilele walikuwa Edmund Hillary wa New Zealand na sherpa Tenzing Norgay wa Nepal tarehe 29 Mei 1953.

[edit] Jina

Wenyeji upande wa Nepal huuita mlima "Sagarmatha" (सगरमाथा Mungu mama wa anga) na majirani upande wa Tibet huuita "Qomolangma" („Mama wa dunia").

Wazungu waliokuwa wa kwanza wa kuchora ramani ya sehemu zile wakauita mwaka 1852 „mlima XV“. Jina la Everest lilianza kutumiwa na Waingereza tangu 1865 kwa heshima ya Sir George Everest aliyekuwa mpimaji mkuu wa ramani wa Uingereza kwa sababu alikuwa ameonyesha bidii kubwa katika upimaji wa Uhindi wa Kiingereza.