User talk:Malangali
From Wikipedia
Malangali, kazi nzuri sana. Tupo pamoja! --Ndesanjo 26 Agosti 2006 (UTC)
Contents |
[edit] Viungo
Malangali, asante kwa orodha ya makabila! Kazi nzuri na msingi bora kwa wengine wanaoweza kuchangia!! Ni vizuri umekumbuka kuanzisha pia "Category". Nimeongeza sasa kiungo kwa "Jamii: Tanzania". Nimejifunza ya kwamba viungo hivi ni muhimu ili makala ipatikane kirahisi. Hata makala kadhaa za kwangu nilizoandika mwanzoni hazionekani tena nisipokumbuka jina kamili kwa sababu sikujali viungo na jamii.
Ukiendelea kutoa michango mema kumbuka na wewe jamii na viungo - kazi isiwe bure! --Kipala 13:41, 25 Agosti 2006 (UTC)
[edit] Majina
Malangali, salamu sana. Umesahihisha majina ya nchi kadhaa katika makala ya "ikweta". Hapa hatuna makubaliano bado katika wikipedia hii. Kuna picha ya kwamba hakuna umoja bado kati ya wazungumzaji na waandishi wa Kiswahili jinsi gani kuandika majina ya nchi. Kuna namna nyingi za kutamka na kuandika. Kwa bahati mbaya kamusi kubwa (kwa mfano za TUKI) zimeacha majina haya kando. Wala hakuna namna moja katika vitabu vya Atlasi zetu nisipokosei.
Mara nyingi katika wikipedia tunafuata ama maandishi jinsi ilivyo katika nchi ile au karibu nayo; kama majina ya Kiswahili ya pekee yapo tunayatumia (Ufaransa, Uingereza); lakini wengine wanapendelea kama wewe kufuata sauti tu. Ila tu ukitaka kutumia maandishi kama "Ekwado" lazima uangalie mambo mawili: a) Je umbo hili linatumia au linakata marejeo kwa makala mengine - b) pili: Je maneno yanayofuata baada ya "Ekwado" katika mabano bado yana maana? Ningeona vema ukitaka kushughulika mambo haya chukua orodha yote ya Amerika Kusini tupate muundo moja. --Kipala 20:40, 22 Juni 2006 (UTC)
- Kipala, asante sana kwa kunikaribisha. Kuhusu majina ya nchi, kuna orodha nzuri inayopatikana kwenye Kamusi Hai. Orodha hii inafuata orodha tatu nyingine: zile za BAKITA, TUKI, na Redio Tanzania Dar es Salaam. Vikundi hivi vitatu vilisanifisha (au viliswahilisha, ukipendelea) majina ya nchi zote za dunia. Kama ulivyosema, mara nyingi hakuna makubaliano baina ya vyanzo mbalimbali, na orodha hiyo ya Kamusi Hai inaonyesha mitafaruku. Lakini kwa jumla orodha ya Kamusi Hai inaonyesha majina yaliyopendekezwa na wataalamu wa vyuo na waandishi wa habari. Je, tufuate mapendekezo haya, au tuhimize istilahi nyingine ya Kiwikipedia? Nafikiri ni afadhali tufuate njia moja na wao waliopewa cheti kusanifisha lugha rasmi, lakini naomba shauri lako.
- Orodha ya TUKI ilichapishwa katika Kamusi ya Kiswahili Sanifu, Toleo la Pili, mwaka 2004, kurasa 473-477. Orodha hii ilifuata mapendekezo rasmi ya orodha ya BAKITA kutoka mwaka 2001, lakini ilibadili maneno mbalimbali (Ekwado badala ya Ikwado, kwa mfano). Baada ya hapo, Redio Tanzania Dar es Salaam ilipendekeza mabadiliko mengine mwaka 2005, kufuatana na matumizi yao. Mapendekezo yote yanaonekana katika orodha ya majina ya nchi iliyoandaliwa na Kamusi Hai ya Kiswahili kwenye Mtandao. Malangali 18:01, 23 Juni 2006 (UTC)
-
- Ndugu Malangali, nashukuru kwa jibu lako. Tunafurahia kila safari jina jipya lapatikana maana tuko wachache mno. Nasita kidogo kujibu namna gani. Kwanza nimefurahi kuona ordoha kwa sababu nimetafuta orodha ya aina hii na sijaikuta (nimewahi kutumia Kamusi Hai mara kadhaa ingawa kwa kusitasita kwa sababu nimeona kasoro mara nyingi; lakini inasaidia ukikaa kwenye kompyuta na kusikia uwivu kutembea tena hatua tano hadi rafu ya vitabu.Ila tu orodha hii sijawahi kukuta). Kwa bahati mbaya Kamusi yangu ya Kiswahili Sanifu ni toleo la kwanza hakuna orodha ya majina ya kijiografia.
-
- Kimsingi nakubali kabisa: tufuate ushauri wa wataalamu. Isipokuwa nikiona orodha hiyo ninasita. Mimi binafsi sipendezwi na mwelekeo wa „kupijinisha“ majina haya yote; yaani kuchukua majina ya asili katika lugha mbalimbali na kuyaandika kufuatana kwa matamshi ya Kiingereza kwa tahajia ya Kiswahili. (jinsi ilivyo kawaida katika lugha zinazoitwa „Pidgin english“ – hivyo kupijinisha). Nikiwa mpenzi wa etimolojia inaniudhi kusaga kila jina nzuri ya asili ya Kiarabu, Kilatini, Kigiriki, Kihindi n.k. kwa masikio ya Mwingereza kwanza na kufinyanga baadaye vumbi yake kwa ulimi wa Mswahili. Habari nyingi zinapotea kwa njia hii (kwa mfano ya kwamba jina la nchi ya Ecuador ni neno „ikweta“ tu kwa Kihispania – Ekwado inafaa kuwa chakula au kinywaji cha Kighana -TULE WAKISHINDA)
-
- Ninasita hasa kufuata orodha hii kwa kwa sababu tatu:
- siamini kweli ya kwamba wasomi wa Kiswahili kutoka Tanzania watakuwa msaada sana katika kujenga wikipedia. Maisha ya TZ ni magumu; msomi mwenye kutumia mitambo hii hatapenda sana kupoteza muda wake kuandika kwa wikipedia kazi isiyo na shukrani wala sifa kwenye chuo kikuu wala haina mapato (sijawahi kupata jibu baada ya jaribio la kuomba msaada kutoka watu mbalimbali huko). Sisi tulivyo ni ama Waswahili hasa wale walio mbali masomoni ya ng’ambo au watu wa nje waliojifunza na kupenda Kiswahili. Ningependa sana tuwe na maprofesa wawili watatu wa TUKI lakini hali halisi naogopa tutategemea kwa muda kidogo watu jinsi walivyo. Ila tujaribu kila namna kukaribisha wenyeji walioko TZ au EAK.
- Ninasita hasa kufuata orodha hii kwa kwa sababu tatu:
-
-
- nina wasiwasi ya kwamba orodha hii itafanya kazi na kusaidia. Wengi watakaotumia wikipedia kwa Kiswahili na kushirikiana kwetu ni watu waliopata elimu yao hasa kwa Kiingereza na lugha za nje; Wakenya kati yetu wanakosa hata masomo ya shule ya msingi kwa Kiswahili. Maana yake ni ya kwamba msamiati si pana sana; tukitumia umbo la kimaandishi ambalo ni mbali sana na yale waliyozoea tunaongeza ugumu wa kutumia wikipedia. Kodivaa, Babadosi au Aminya haisaidii bali kuleta ugumu. Sisomi hapa magazeti ya Tanzania: Je, wanafuata orodha hii au kwa kiasi tu? Kenya hawafuati – ni gazeti moja tu kwa Kiswahili.
-
-
-
- HASA sababu ya tatu ni: je,orodha hizi zinatosha kwa matumizi yetu? Nimetunga sasa sehemu kubwa ya makala ya nchi za Afrika (nadhani ziko kwenye orodha). Niko kwa miji mikuu (je, ziko zote katika orodha ya TUKI ???) pamoja na miji mingine na mito. Majina mengi wazee wa TUKI hawakuwahi kuangalia bado. Kama wikipedia hii inaendelea kupanuka jinsi ilivyo hata na watu wachache tunaendelea kilasiku kutaja majina yasiyopo kwenye orodha za TUKI n.k. Je tufanye nini? Kusubiri?
-
-
-
- Pendekezo langu: tusipoteze muda wetu kusahihishana (isipokuwa kama sahihisho la mtu mgeni inaharibu viungo kati ya makala) lakini tuendelee kushauriana. Kwa sasa tutumie mbinu za mtandao na hasa „mielekezo“: Ukipenda sana „Kodivaa“ lakini makala ya „Cote d’Ivoire“ iko tayari: andika makala fupi ya „REDIRECT“. Vilevile kama wewe umeandika makala ya „Ekwado“ mimi ningeweka REDIRECT nikitumia Ecuador. Mtandao na mitambo inatupa kiwango hiki cha uhuru.
-
-
- Unaonaje? --Kipala 20:48, 23 Juni 2006 (UTC)
[edit] Afrophonewikis
Hujambo, Malangali. It took me some time, but I have finally become a member of the Afrophonewikis Group following your request to do so at my English talk page. Thanks for the heads up, I think the formation of this group is a step in the right direction. — mark ✎ 17:51, 26 Septemba 2006 (UTC)
[edit] Wabunge
Malangali, hongera kwa makala za Wabunge na asante kwa kazi kubwa!! Je unaonaje kama ungeingiza pia chama na hasa jimbo la uchaguzi? Tovuti la bunge lina maelezo haya na ingeboresha wikipedia yetu kwa ujumla kwa sababu tunapata nafasi ya viungo. Mfano: Juma Jamaldin Akukweti ni Mbunge katika Bunge la Tanzania. Alichaguliwa katika jimbo la Tunduru ni mwanachama wa CCM.
Najua ni kazi hasa kwa sababu ya idadi kubwa ya makala lakini ukianza hivyo kwa wabunge utakaoweka? Pia nimeona tatizo la jamii "wanasiasa wa tanzania" iliyokuwa na REDIRECT kwa "wanasiasa Tanzania" hivyo wabunge hawakuonyeshwa. Nimetenganisha na kuwaweka zote mbili chini ya "watu wa Tanzania". Ukiwa na nafasi labda chungulia na kuhamisha wale wachache wa jamii "wanasiasa Tanzania" katika jamii uliotumia? --Kipala 20:44, 29 Novemba 2006 (UTC)
-
- Asante, Bw. Kipala. Kwa sasa, naona ni rahisi zaidi nikianzisha mbegu bila kuweka maarifa kama jimbo la uchaguzi. Ninachofanya naweza kufanya chapuchapu nikitumia mikasi na gundi. Baadaye itabidi kurudi kwenye kurasa za kila Mbunge na kuweka majimbo, siku za kuzaliwa, nk, lakini mwanzonimwanzoni napendelea kufanya bila kurudia kila mara kwenye dirisha jingine. Kama kuna mwengine anayetaka kufanya kama unavyopendekeza, lakini, karibu sana - wako zaidi ya Wabunge 300! :) Malangali 21:49, 1 Desemba 2006 (UTC)
[edit] Re: Vandalism
Hi Malangali, please see this page for more information on page protection. And here's a link to view the current protection level for Mpira wa miguu. Link --Az1568 04:01, 12 Desemba 2006 (UTC)
- Since all your vandals on the page Mpira wa miguu are IP addresses, selecting "registered user only" will allow real users to make legitimate edits to the page but keep the IP spammers away. Also, check to see if the IPs are open proxies (en:open proxy). If they are, they may be indefinately blocked (m:WM:NOP).
- English WpA uses www.completewhois.com/rbl_lookup.htm to test for proxies. As an example, the first vandal to that page, User:69.74.139.149 is definately a proxy: www.completewhois.com/cgi-bin/rbl_lookup.cgi?query=69.74.139.149&display=webtable, likewise, so is User:80.75.0.253: www.completewhois.com/cgi2/rbl_lookup.cgi?query=80.75.0.253&display=webtable. Also check the IPs reputation on larger WMF wikis. For example User:83.143.18.69 has been blocked as an open proxy/zombie on the eN WpA: en:User talk:83.143.18.69. Similarly User:213.42.21.77 is definately block-worthy: www.completewhois.com/cgi2/rbl_lookup.cgi?query=213.42.21.77&display=webtable, User:81.21.176.10 is a Email and wiki SPAMmer: www.completewhois.com/cgi2/rbl_lookup.cgi?query=81.21.176.10&display=webtable , User:65.198.48.23 is evidently not a proxy, but has made repetitive robotic edits to other wikis. I'll try and remember to check back to this page, so you can ask questions here, or on my eN wikipedia talk page (en:User_talk:68.39.174.238). 68.39.174.238 03:53, 16 Desemba 2006 (UTC)