Utumwa

From Wikipedia

Utumwa ni mfumo unaotoa fursa kwa binadamu kummiliki binadamu mwenzake. Binadamu anayemilikiwa anakuwa na hadhi sawa na chombo au kifaa chochote kinachoweza kuuzwa.

Mfumo huu ulikuwa maarufu kabla ya harakati za ukoloni duniani mathalani karne ya 15 ambapo watumwa walihitajika katika shughuli zakilimo na uchimbaji madini katika sehemu mbalimbali za ulimwengu.

Mfumo huu uunda matabaka ya "mabwana" ambao humiliki watumwa na "watwana" ambao ni watumwa wenyewe.