Samoa
From Wikipedia
|
|||||
Wito la taifa: Fa'avae i le Atua Samoa (Samoan: "Samoa is founded on God") |
|||||
Wimbo wa taifa: The Banner of Freedom | |||||
![]() |
|||||
Mji mkuu | Apia |
||||
Mji mkubwa nchini | Apia | ||||
Lugha rasmi | Samoan, Kiingereza | ||||
Serikali
O le Ao o le Malo
|
Parliamentary democracy Malietoa Tanumafili II |
||||
Uhuru Tarehe |
1 Januari 1962 | ||||
Eneo - Jumla - Maji (%) |
2,831 km² (174 ya) 0.3% |
||||
Idadi ya watu - Julai 2005 kadirio - Msongamano wa watu |
185,000 (185 ya) 65/km² (126 ya) |
||||
Fedha | Tala (WST ) |
||||
Saa za eneo - Kiangazi (DST) |
(UTC-11) (UTC) |
||||
Intaneti TLD | .ws | ||||
Kodi ya simu | +685 |
Samoa ni nchi ya visiwani ya Polynesia katika Pasifiki ya kusini yenye wakazi 176,710 (2001 sensa). Nchi huru ya Samoa ni sehemu ya magharibi ya funguvisiwa ya Samoa. Sehemu ya mashariki iko chini ya Marekani.
[edit] Jiografia
Eneo lake ni visiwa tisa (au kumi: kama kisiwa kidogo sana kinahesabiwa humo) jumla kilomita za mraba 2,934. Visiwa viwili vikubwa vya Upolu (1,118 km²) na Savai'i (1,708 km²) vina asilimia 96 za eneo lote. Kuna bado visiwa viwili vidogo vya Manono na Apolima vyenye wakazi halafu visiwa vingine visivyokaliwa na watu.
Mji mkuu wa Apia uko Upolu.
Mahali pa juu ni mlima Mauga Silisili mwenye kimo cha mita 1,858.
[edit] Historia
Samoa ilikuwa ufalme wa kujitegemea kabisa hadi 1889. Mwaka ule uliwekwa chini ya ulinzi wa nchi tatu za Uingereza, Ujerumani na Marekani. Baada ya kifo cha mfalme 1898 kulitokea fitina juu ya mfuasi wake na nchi za nje zilingia katia. Mkataba wa Berlin wa 1890 iligawa funguvisiwa ya Samoa kati ya Ujerumani na Marekani. Sehemu ya magharibi ikawa "Samoa ya Kijerumani".
Wakati wa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia visiwa vilitekwa na New Zealand vikabaki chini ya nchi hiyo kama maeneo yaliyokabidhiwa na Shirikisho la Mataifa na baada ya 1945 na Umoja wa Mataifa kwa jina la "Samoa ya Magharibi".
Uhuru ulipatikana mawka 1962.
![]() |
Makala hiyo kuhusu "Samoa" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri". Ikiwepo makala kuhusu Samoa kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili. |