Juba (mto)
From Wikipedia
Mto wa Juba | |
---|---|
Chanzo | Maungano ya mito ya Dawa na Gebele, Ethiopia |
Mdomo | Bahari ya Hindi kaskazini ya Kismayu |
Nchi | Ethiopia, Somalia |
Urefu | 1,659 km |
Kimo cha chanzo | ? m katika milima ya Bale, Ethiopia |
Mkondo | ? m³/s |
Eneo la beseni | 497,626 km² |
Juba (pia: Jubba, Giuba, Ganane au Genale) ni mto mkubwa wa Somalia mwenye maji mwaka wote. Chanzo chake ni katika nyanda za juu za Ethiopia. Unafika Bahari ya Hindi karibu na mji wa Kismayu.
Wakati wa ukoloni mto Juba ulikuwa mpaka kati ya Kenya na eneo la Somalia lililokuwa chini ya koloni la Italia. Mwaka 1925 Uingereza iliwaachia Waitalia eneo la nchi kusini mwa mto (kiit.: Territorio dell'Oltre Giuba -kiing.: Jubaland)