Agano la Kale

From Wikipedia

Agano la Kale ambalo hujulikana pia kama Biblia ya Kiebrania ni mkusanyiko wa vitabu vya sehemu ya kwanza ya Biblia inayotumiwa na waumini wa Kikristo duniani na pia kwa kiasi fulani waumini wa Kiislamu. Mkusanyiko huu umegawanywa katika makundi ya sheria, historia, ushairi, na unabii. Vitabu vya Agano la Kale viliandikwa kabla ya kuzaliwa kwa Yesu.

Kwa mujibu wa wana historia wa Biblia, vitabu vya Agano la Kale viliandikwa kati ya karne ya 5 KK na karne ya pili KK. Hata hivyo inaaminika kuwa vitabu viitwavyo, Vitabu vya Musa, na Wimbo wa Debora viliandikwa nyuma zaidi.

[edit] Viungo vya nje

Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Agano la Kale" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Agano la Kale kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.