Mwewe

From Wikipedia

Mwewe
Mwewe domo-njano
Mwewe domo-njano
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Falconiformes (Ndege kama kozi)
Familia: Accipitridae (Ndege walio na mnasaba na mwewe)
Jenasi: Chelictinia Lesson, 1843

Elanoides Vieillot, 1818
Elanus Savigny, 1809
Gampsonyx Vigors, 1825
Haliastur Selby, 1840
Harpagus Vigors, 1825
Ictinia Vieillot, 1818
Lophoictinia Kaup, 1847
Machaerhamphus Bonaparte, 1850
Milvus Lacépède, 1799 Rostrhamus Lesson, 1830

Mwewe ni ndege mbua wa jenasi mbalimbali (angalia sanduku ya uainishaji) ya familia Accipitridae. Hawana sifa bainifu pamoja isipokuwa wengi wana mkia mwenye panda. Mabawa yao ni marefu na miguu yao haina nguvu kwa sababu yake ndege hawa hupuruka sana. Hukamata aina nyingi za mawindo, kama wanyama wadogo, ndege na wadudu wakubwa, lakini hula mizoga sana.

[edit] Spishi za Afrika

  • Chelictinia riocourii, Mwewe Kizelele (Scissor-tailed or African Swallow-tailed Kite)
  • Elanus caeruleus, Mwewe Kipupwe (Black-winged Kite)
  • Machaerhamphus alcinus, Mwewe Mlapopo (Bat Hawk)
  • Milvus migrans, Mwewe Domo-jeusi (Black-billed Kite)
  • Milvus milvus, Mwewe Mwekundu (Red Kite)
  • Milvus parasiticus, Mwewe Domo-njano (Yellow-billed Kite)

[edit] Spishi za mabara mengine

[edit] Picha