Las Palmas de Gran Canaria

From Wikipedia

Kanisa Kuu la Santa Ana
Kanisa Kuu la Santa Ana
Mapwa ya Las Canteras
Mapwa ya Las Canteras
Mahali pa Las Palmas kisiwani

Las Palmas de Gran Canaria (kifupi: Las Palmas) ni mji wa Hispania katika kaskazini-mashariki ya kisiwa cha Gran Canaria mwenye wakazi 376,953 (2004). Las Palmas ni makao makuu ya utawala wa kisiwa cha Gran Canaria na moja kati ya miji mikuu miwili ya funguvisiwa ya Visiwa vya Kanari inayojitawala ndani ya Hispania. Visiwa vya Kanari vimo katika sehemu ya Kiafrika ya Atlantiki. Tangu 1982 ni mji mkuu pamoja na Santa Cruz de Tenerife. Kila baada ya miaka minne mmoja kati ya miji hii miwili una nafasi ya kuwa mji mkuu.