Afrika ya Mashariki ya Kiingereza

From Wikipedia

Stempu ya posta ya 2 1/2 anna, 1896
Stempu ya posta ya 2 1/2 anna, 1896

Afrika ya Mashariki ya Kiingereza ilikuwa jina kwa ajili ya eneo la Kenya lililowekwa chini ya utawala wa ulinzi wa Uingereza wakati wa miaka 1895 hadi 1920 BK.

Wakati wa mashindano ya kugawa Afrika kati ya madola ya Ulaya ndiyo Kampuni ya Kifalme ya Kiingereza kwa Afrika ya Mashariki ilianza shughuli zake katika eneo hili kwa kibali cha sultani ya Zanzibar kuanzia mwaka 1888. Kampuni ilitakiwa kuwa na mamlaka juu ya eneo hili kwa kusudi la kufanya biashara lakini uwezo wake haukutosha kutimiza shughuli hasa maandalizi ya kujenga reli ya Uganda kati ya Mombasa na Kampala.

Baada ya azimio la kujenga reli Uingereza iliona haja ya kulinda eneo la reli hiyo ikatangaza eneo lote kati ya Mombasa na Uganda kuwa chini ya ulinzi wake kuanzia tar. 01.07.1895. Hivyo mipango ya kujenga reli ilikuwa mwanzo wa koloni ya Afrika ya Mashariki ya Kiingereza iliyokuwa Kenya baadaye. Eneo la utawala wa kiingereza lilipanushwa zaidi hadi kukutana na maeneo chini ya utawala wa Italia (Somalia) na Ethiopia upande wa Kaskazini na eneo chini ya utawala wa ushirikiano wa Misri na Uingereza (Sudan). Upande wa kusini mpaka ulifuata mapatano na Afrika ya Mashariki ya Kijerumani.

Mpaka na eneo chini ya utawala wa ulinzi wa Uganda ulisahihishwa mwaka 1905; hadi wakati ule sehemu kubwa ya eneo la Kenya ya Magharibi ya leo ilihesabiwa kuwa upande Uganda.

Baada ya vita kuu ya kwanza hali ya eneo lilibadilishwa kuwa koloni ya Kenya kuanzia 1920.


Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Afrika ya Mashariki ya Kiingereza" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Afrika ya Mashariki ya Kiingereza kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.

Lugha nyingine