Mtori

From Wikipedia

Mtori:

Ni chakula ambacho kinapendwa na wachagga wengi na hupenda kula hasa wakati wa usiku ingawa leo mijini wengi hupendelea kula wakati wa asubuhi zaidi. Na vile vile ni chakula cha wagojwa hasa wale wasioweza kula chakula kigumu.

Matayarisho ya Mtori:

-Ndizi mshare au ndizi ng'mbe -Nyama hasa ya utumbo -Sowe ( inatokana na viazi vyenye asili ya magimbi)/ viazi mviringo -Vitunguu -Nyanya -Chumvi

Utengenezaji:

Nyama hupikwa mpaka kuwa laini na pia kupata supu ambayo itatumika wakati wakupoonda ndizi. Pia ndizi hupikwa pamoja na vitinguu na nyanya mpaka kuwa laini kabisa.Baada ya hapo maji yakikaauka ndizi hizo hupondwa pondwa mpaka kuwa kama ugali.Sasa supu iliobaki kwenye nyama inachanganywa na ndizi zilizopondwa mpaka kupata kitu kama uji ambao ni mtori. Tayari kwa matumizi hasa hasa ikiwa bado moto.