Wagadugu

From Wikipedia

Barabara katika kitovu cha Wagadugu karibu na uwanja wa Umoja wa Mataifa.
Barabara katika kitovu cha Wagadugu karibu na uwanja wa Umoja wa Mataifa.

Wagadugu (kifaransa Ouagadougou) ni mji mkuu wa Burkina Faso pia mji mkubwa kabisa wa nchi hiyo. Mwaka 2005 idada ya wakazi ilikuwa milioni 1,2. Mji unakua haraka.

Wagadugu iko katika jimbo la Kadiogo. Kuna ofisi za serikali na viwanda kadhaa za za nguo na vyakula.

Mji ni pia kitovu cha usafiri na mawasiliano. Kuna kiwanja cha kimataifa cha ndege na njia ya reli kwenda Abidjan (Côte d'Ivoire), halafu barabara za kwenda Lome (Togo), Bamako (Mali), Niamey (Niger), Accra (Ghana).

Wagadugu ina chuo kikuu kilichokuwa chuo cha mwanahistoria maarufu Joseph Ki-Zerbo. Tamasha la kimataifa la filamu za Afrika (FESPACO) hufanyiwa Wagadugu.

Meia ya mji ndiye Simon Compaoré liyechaguliwa 1995.