Antili za Kiholanzi

From Wikipedia

Nederlandse Antillen
Antili za Kiholanzi
Flag of Antili za Kiholanzi Image:Nantillescoa.png
Bendera Nembo
Wito la taifa: Libertate unanimus
(Kilatini: "Umoja kwa uhuru")
Wimbo wa taifa: Our islands in the sea
Lokeshen ya Antili za Kiholanzi
Mji mkuu Willemstad (Curacao)
12°7′ N 68°56′ W
Mji mkubwa nchini Willemstad (Curacao)
Lugha rasmi Kiholanzi
Serikali
Malkia
Gavana
Waziri Mkuu

Beatrix wa Uholanzi
Frits Goedgedrag
Emily de Jongh-Elhage
Ufalme wa kikatiba
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
960 km² (ya 184)
Idadi ya watu
 - Julai 2005 kadirio
 - Msongamano wa watu
 
183,000 (ya 185)
229/km² (ya 51)
Fedha Gulden ya Antili za Kiholanzi (ANG)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
(UTC-4)
(UTC)
Intaneti TLD .an
Kodi ya simu +599
Map of the Netherlands Antilles
Map of the Netherlands Antilles


Antili za Kiholanzi ni visiwa katika Bahari ya Karibi kati ya Puerto Rico na pwani la Venezuela (Amerika Kusini) vinavyohesabiwa kati ya visiwa vya Antili Ndogo. Visiwa vitano hukaliwa na watu kuna vingi vingine vidogo. Vyote vilikuwa koloni za Uholanzi vimekuwa sehemu za Ufalme wa Uholanzi katika hali mbalimbali za kisheria.

Visiwa hivi ni:

  • Visiwa vya Leeward ("pasipo na upepo") viko karibu na pwani la Venezuela
    • Bonaire
    • Curaçao
    • Aruba

Vyote vitatu vimeondoka katika Umoja wa Antili za Kiholanzi uliopatikana hadi Oktoba 2006. Visiwa hivi vikubwa kiasi vimepata hali kama nchi ndani ya Ufalme wa Uholanzi; kila nchi ina bunge na serikali yake. Siasa ya nje na mambo ya jeshi ni ya pamoja zikiendeshwa na serikali ya Den Haag. Mahakama Kuu ya Den Haag itakuwa mahakama ya pamoja kwa ajili ya Uholanzi, Aruba, Curacao na Bonaire.

Nyumba katika bandari ya Willemstad (Curacao)
Nyumba katika bandari ya Willemstad (Curacao)
  • Visiwa vya Windward ("penye upepo") viko karibu na Puerto Rico
    • Saba
    • Sint Eustatius oder, wie die Einheimischen sagen, Statia.
    • Sint Maarten (kusini ya kisiwa pekee; kaskazini ni eneo la Ufaransa chini ya mkoa wa Guadeloupe)

Visiwa hivi vitatu vitahesabiwa kama miji ya Uholanzi. Wakazi watapigia kura bunge la Uholanzi na bunge la Ulaya.

Antili za Kiholanzi zitakwisha kama kitengo cha utawala ndani ya Ufalme wa Uholanzi kuanzia 1 Julai 2007.