Nyanda za Juu za Bie

From Wikipedia

Nyanda za Juu za Bie ziko kwenye kitovu cha nchi Angola. Zinapanda hadi ya kuwa na kimo cha 2,619 m juu ya UB.

Kutokana na kiasi kikubwa cha mvua kinachopatikana hapa eneo ni chanzo cha mito mingi muhimu ya Afrika ya Kusini na Afrika ya Kati.

[edit] Mito muhimu inayoanza Nyanda za Juu za Bie

  • Kwanza (Cuanza) - inaelekea kaskazini - magharibi na kuishia Atlantiki
  • Kasai inaelekea kaskazini na kuishia mto Kongo
  • Kwango inaelekea kaskazini na kuishia kwenye mto Kasai ndani ya Kongo.
  • Kwando (Cuando) - inaelekea kusini-mashariki na kuishia Zambezi
  • Kubango-Okavango - inaelekea kusini halafu kusini-mashariki na kuishia Delta ya Okavango kwenye Kalahari
  • Kunene (Cunene) - inaelekea kusini-magharibi na kuishia Atlantiki mpakani na Namibia.
  • kuelekea magharibi ni mito midogo tu
  • Zambezi ikitokea kaskazini inapita karibu na Nyanda za Juu za Bie na kupokea sehemu ya maji yake hapa.


Mji mkubwa katika eneo ni Huambo (zamani: Lisbon mpya)

Lugha nyingine