Wabukusu
From Wikipedia
Wabukusu ni kati ya koo kubwa za Waluhya (Abaluhya) katika magharibi ya Kenya na mashariki-kusini ya Uganda kwenye mitelemko ya mlima Elgon. Eneo lao katika Kenya ni hasa wilaya ya Bungoma (Mkoa wa Magharibi). Wako pia Kitale huko mkoa wa Bonde la Ufa.
Idadi yao ilikadiriwa kuwa karibu lakhi sita mwaka 1987.
Wakati wa kuja kwa ukoloni Wabukusu walijaribu kuwazuia Waingereza. Mwaka 1895 walijitetea katika Boma la Chetambe karibu na Bungoma lakini walishindwa na silaha kali za Waingereza.
Upinzani ulirudiwa katika miaka ya 1940 na 1950 Wabukusu wengi walipomfuata Elijah Masinde na jumuiya yake ya Dini ya Musambwa.
![]() |
Makala hiyo kuhusu "Wabukusu" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri". Ikiwepo makala kuhusu Wabukusu kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili. |