Austen Chamberlain
From Wikipedia
Austen Chamberlain (16 Oktoba, 1863 – 16 Machi, 1937) alikuwa mwanasiasa kutoka nchi ya Uingereza. Kuanzia 1924 hadi 1929 alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje. Mwaka wa 1925, pamoja na Charles Dawes alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel kwa Amani kwa ajili ya kazi yake ya kupitisha Maafikiano ya Lokarno.