Kanuni ya Pauli
From Wikipedia
Kanuni ya Pauli ilitangazwa mwaka wa 1925 na Wolfgang Pauli. Inahusu elektroni za atomu. Kila elektroni ina tarakimu nne za kwanta. Kanuni ya Pauli inadai kwamba tarakimu hizo nne haziwezekani kuwa sawa kwa elektroni mbili ndani ya atomu moja.