9 Novemba
From Wikipedia
[edit] Matukio
- 694 - Mfalme Egica, mfalme wa WaVisigoth wa Hispania, anawashtaki Wayahudi kuwasaidia Waislamu, na anawaadhibu kuwa watumwa.
- 1282 - Papa Martin IV anamtenga Mfalme Peter III wa Aragon na kanisa.
- 1494 - Akina de Medici wanaanza kuwa watawala wa mji wa Florence.
- 1799 - Napoleon Bonaparte anapindua serikali ya Ufaransa.
- 1848 - Robert Blum anauawa katika mji wa Vienna.
- 1872 - Moto unateketeza sehemu kubwa ya mji wa Boston.
- 1918 - Mfalme Mkuu Wilhelm II wa Ujerumani anajiuzulu, na Ujerumani unatangazwa kuwa jamhuri.
- 1938 - Usiku wa Chembechembe (kwa Kijerumani: Reichskristallnacht), ambapo WaNazi wanatumia nguvu na vurugu dhidi ya Wayahudi.
- 1989 - Nchi ya Ujerumani wa Mashariki inafungulia Ukuta wa Berlin na kuwaruhusu wananchi wake kusafiri bila shida kwenda Ujerumani wa Magharibi.
[edit] Waliozaliwa
[edit] Waliofariki