Zauditu wa Uhabeshi

From Wikipedia

Zauditu (29 Aprili, 18762 Aprili, 1930) alikuwa malkia mtawala wa Uhabeshi kuanzia 27 Septemba 1916 hadi kifo chake. Alimfuata Iyasu V. Jina lake la kubatizwa lilikuwa Askala Maryam. Alikuwa mtoto wa kwanza wa Menelik II. Mwanzoni utawala wake ulisumbuliwa na uasi wa Iyasu aliyekuwa ameuzuliwa. Malkia huyu anajulikana kwa jinsi alivyopenda dini na alivyokuwa mpinzani mkubwa wa mabadiliko aliyokuwa akiyafanya Ras Tafari Makonnen. Zauditu aligombana sana naye Makonnen, kuhusu mambo ya siasa lakini alishindwa. Naye Tafari alimfuata kama mfalme chini ya jina la Haile Selassie.

Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Zauditu wa Uhabeshi" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Zauditu wa Uhabeshi kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.