Muhimbili
From Wikipedia
Muhimbili ni taasisi kubwa ya afya na elimu ya afya iliyoko Dar es Salaam Tanzania.
Kama Chuo cha Elimu ya Afya ni sehemu ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Ndani ya chuo kuna idara nne na taasisi tano.
Idara nne ni kama zifuatazo:
- Idara ya utaalamu wa meno
- Idara ya uganga
- Idara ya uuguzi
- Idara ya madawa
Kati ya taasisi kuna taasisi za afya ya umma na uganga wa kimila.
Muhimbili ilianzishwa mwaka 1963 ndani ya hospitali iliyoitwa Princess Margaret Hospital na wanafunzi 10 waliofuata kozi za uganga au upasuaji.
Neno Muhimbili limetokana kwa kizaramo "mibili" likimaanisha kiungo cha mtoto tumboni na mama yake (plasenta) Hospitali ilipoanza wazaramo walisema "hapo ndipo wanawake wanapoenda kuacha mibili yao". Neno Muhimbili likazaliwa nalo ladumu hadi leo.
Kwa leo hii Muhimbili ina shule ya madaktari, wauguzi, mafamasia, waganga wa meno, mabwana afya, mabwana mazingira na elimu ya juu ya afya.