Gustav Stresemann
From Wikipedia
Gustav Stresemann (10 Mei, 1878 – 3 Oktoba, 1929) alikuwa mwanasiasa kutoka nchi ya Ujerumani. Mwaka wa 1923 alikuwa Waziri Mkuu na kuanzia 1924 hadi 1929 alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje. Mwaka wa 1926, pamoja na Aristide Briand alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel kwa Amani.