Mkoa wa Kaskazini-Mashariki (Kenya)
From Wikipedia
Kaskazini-Mashariki ni moja kati ya mikoa 9 ya Kenya. Eneo lake ni 127 000 km² [1] kuna wakazi 962,143 (sensa ya 1999).
Wakati wa ukoloni eneo hili liliitwa "Northern Frontier District" (Eneo la mpakani wa kaskazini) likitawaliwa pekee na sehemu kubwa ya Kenya. Wakazi walio wengi ni Wasomalia kilugha na kiutamaduni; kuwepo kwao ndani ya Kenya badala ya Somalia ni urithi wa mipaka ya kikoloni. Wengine ni Waborana, Warendille na Waturkana. Kuna pia makambi makubwa ya wakimbizi Wasomalia hasa karibu na Daadab.
[edit] Hali ya hewa
Eneo hili ni kavu sana. Mbali na bonde la mto wa Tana na maeneo mengine madogo mkoa haufai kwa kilimo. Wakazi walio wengi hujipatia riziki kutokana na ufugaji.
[edit] Utawala
Mkoa wa Kaskazini-Mashariki una wilaya nne:
- Garissa -- makao makuu Garissa
- Ijara -- makao makuu Ijara
- Wajir -- makao makuu Wajir
- Mandera -- makao makuu Mandera
|
![]() |
---|---|
Bonde la Ufa | Kaskazini-Mashariki | Kati | Magharibi | Mashariki | Nairobi | Nyanza | Pwani| |