Wikipedia talk:Jumuia
From Wikipedia
[edit] Dini na Historia
Sielewi namna gani makala ya "Historia" ina lugha ya kidini?? - Kipala
- Hiyo ilikuwa zamani kidogo. Sasa haina lugha ya kidini tena. Kwa hiyo sasa nimefuta mtajo wa makala ya "Historio" katika ukarasa huu. Marcos 23:12, 2 Februari 2006 (UTC)
[edit] Communist Manifesto
Ningependa msaada wenu kutafuta nakala ya "Communist Manifesto" kwenye lugha ya Kiswahili. Sina uhakika kama imewahi kutafsiriwa. Yeyoe anaefahamu iwapo inapatikana kwenye mtandao anielekeze jinsi ya kuipata. Kama haiipo basi yeyote apendae kushirikiana kuichapisha anaweza kunitumia barua pepe: khalyboy@hotmail.com
Ahsante Khalid
[edit] Msaada wa kupakua picha "commons"
Marcos na Matt, hamjambo? Kuhusu kupakua na kupakia picha: ninaona mara kwa mara ya kwamba picha, ramani n.k. haimo Commons nikitaka kuichukua kutoka wiki nyingine. Sas sijaelewa jinsi gani kuihamisha huko. Je, mnaweza kuweka kiungo cha kudumu mahali? au kuunda fomu? Au angalau kuandika anwani mahali ili ninakili tu?
Yaani nikiona katika, tuseme: en.wikipedia.org picha fulani. Nataka kuichukua kwa makala ya Kiswahili. Kwa kawaida naingia "hariri/edit", nakili mstari wa [[Image:..... na kuiingiza katika makala ya Kiswahili. Nikibonyeza "Mandhari ya mabadilisho" inaonekana au la. Sasa lkuna njia ya kuihamisha commons moja kwa moja? --Kipala 15:06, 14 May 2006 (UTC)
- Ili kupakia picha katika Wikipedia ya Kiswahili, lazima kwanza uihifadhi picha hiyo katika kompyuta yako. Baada ya kuihifadhi katika kompyuta yako, ubofye "Pakia faili" huku kushoto (chini ya "vifaa"). Halafu uchague faili ya picha katika kompyuta yako, ukabofye "upload".
- Umenielewa? Marcos 12:21, 15 May 2006 (UTC)
-
- Asante kwa jibu, Marcos. Njia unayoeleza mimi natumia mara kwa mara. Lakini Matt aliniambia mara kadhaa ni afadhali kama tuweke picha moja kwa moja commons. Alifyeka mara nyingi baada ya mimi kupakia akahamisha picha commons na kuzifuta hapa sw. Swali langu ni kuhusu commons, njia nyingine nimeshaelewa. --Kipala 12:28, 15 May 2006 (UTC)