Mkoa wa Unguja Kaskazini

From Wikipedia

Mkoa wa Kaskazini Unguja, Tanzania
Mkoa wa Kaskazini Unguja, Tanzania

Mkoa wa Kaskazini Unguja ni moja kati ya mikoa 26 ya Tanzania. Iko Unguja kisiwani ambayo ni kisiwa kikubwa cha Jamhuri ya Watu wa Zanzibar.

Makao makuu ya mkoa uko Mkokotoni. Kuna wilaya mbili za Kaskazini Unguja 'A' na Kaskazini Unguja 'B'.

Eneo la mkoa ni 470 km² kuna wakazi 136,953 wakiwemo Kaskazini 'A' 84,348 na Kaskazini 'B' 52,605. Wengi wanajishughulisha na uvuvi na kilimo. Sehemu ya mashariki ya mkoa kuna kilimo cha karafuu. Upande wa magharibi utalii umeanza kuwa muhimu. Eneo la Ras Nungwi ni sehemu moja penye mahoteli ya watalii wa nje.

Kisiwa cha Tumbatu ni sehemu ya mkoa huu.

Miji ya mkoa ndiyo Mkokotoni, Mahonda na Gamba.

[edit] Viungo vya nje

Dira mikoani: Kaskazini Unguja

Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Mkoa wa Unguja Kaskazini" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Mkoa wa Unguja Kaskazini kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.


 
Mikoa ya Tanzania
Bandera Tanzania
Arusha | Dar es Salaam | Dodoma | Iringa | Kagera | Kigoma | Kilimanjaro | Lindi | Manyara | Mara | Mbeya | Morogoro | Mtwara | Mwanza | Pemba Kaskazini | Pemba Kusini | Pwani | Rukwa | Ruvuma | Shinyanga | Singida | Tabora | Tanga | Unguja Kaskazini | Unguja Kusini | Unguja Mjini Magharibi |
Lugha nyingine