Talk:Iceland

From Wikipedia

Kamusi ya "Kamusi Project" inaandika kwamba jina la Kiswahili la nchi hii ni Aisilandi (au Isilandi). Kwa hiyo naania kwamba tuihamishe makala hii iwe "Aisilandi" au "Isilandi". Je, ninyi mnakubali? Marcos 19:33, 22 Julai 2006 (UTC)

Kamusi Project ni mradi mwenye mambo mazuri lakini pia kasoro. Kuhusu orodha iliyoko nyuma yake tumewahi kujadiliana. Mimi sikumbuki kuona "Aisilandi" au kitu kama hiki kamwe. Kama imetajwa gazetini nakumbuka "Iceland". Nisipokosei kuna mapendekezo kadhaa katika orodha hizi ambazo hazikuwahi kutumika; hasa kama ni mahali pasipojadiliwa katika maandiko au magazeti ya Kiswahili majina yale ni nadharia tupu tu. Ni tofauti kuhusu nchi zinazojadiliwa hali halisi. Mimi naona tusipoteze muda kuchezacheza habari za majina haya, tuongeze viungo na tuendelee kujenga kamusi. --Kipala 23:39, 22 Julai 2006 (UTC)