Joseph Erlanger
From Wikipedia
Joseph Erlanger (5 Januari, 1874 – 5 Desemba, 1965) alikuwa daktari na mwanafiziolojia kutoka nchi ya Marekani. Hasa alichunguza elimu ya neva. Mwaka wa 1944, pamoja na Herbert Spencer Gasser alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Tiba.