Vyama vingi vya siasa Tanzania
From Wikipedia
Tanzania ni nchi yenye mfumo wa vyama vingi vya siasa uliorejeshwa katika katiba ya Tanzania mwaka 1992. Chama tawala ni Chama cha Mapinduzi (CCM) ambacho kinatokana na muungano kati ya Tanganyika African National Union (TANU) na Afro Shiraz Party (ASP) ya Zanzibar.
Vyama vingine vya siasa Tanzania ni Civic United Front (CUF), Tanzania Labour Party (TLP), Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), National Convention for Constitution and Reconstruction-Mageuzi (NCCR-Mageuzi), National League of Democracy (NLD), Democratic Party (DP), na Demokrasia Makini.