Songwe (mto)

From Wikipedia

Songwe ni jina la mito miwili ya Tanzania katika mkoa wa Mbeya.

Songwe ya Kaskazini ina chanzo chake katika milima ya Umalila karibu na Santilya iliyopo kusini ya Mbeya ikielekea kaskazini na kuishia Ziwa la Rukwa. Bonde lake limejulikana kati ya wataalamu wa akiolojia kwa mifupa na mabaki ya nyakati za kale zinazopatikana hapa. Barabara ya Mbeya kwenda Zambia inavuka Songwe penye kiwanda cha saruji inayotumia mawe ya bonde la mto. Mto unapita baadaye karibu na kijiji cha Galula kablaya kufikia ziwa Rukwa.

Songwe ya Kusini ina chanzo chake katika milima ileile karibu na Santilya ikielekea kusini na kuishia Ziwa Nyasa. Baada ya kupita Itumba (Ileje) mto ni mpaka kati ya Tanzania na Malawi.

Tabia yake ya kubadilisha-badilisha mwendo wake imesababisha matatizo kati ya nchi jirani kwa sababi mashamba ya watu yamepatikana mara upande moja mara upande mwingine wa mpaka wa kimataifa.


[edit] Viungo vya nje

Taarifa kuhusu Songwe ya kusini mpakana katiy a Malawi na Tanzania (Kin) [1] [2]

Habari za kiakiolojia kutoka bonde la Songwe ya kaskazini