Alfred Nobel

From Wikipedia

Alfred Nobel (21 Oktoba, 183310 Desemba, 1896) alikuwa mhandisi na mwenye viwanda wa nchi ya Sweden. Mwaka wa 1867 aligundua jinsi ya kutengeneza baruti kali. Pia aliboresha utoneshaji wa mafuta. Akafaulu kiuchumi akawa mtajiri na wakati uleule mwenye wasiwasi kuhusu matumizi ya baruti aliyogundua kwa sababu aliona matumizi mabaya kwa ajili ya silaha. Katika hati yake ya wasia alianzisha Tuzo ya Nobel kwa ajili ya mafanikio ya kisayansi lakini pia kwa ajili ya amani duniani.

Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Alfred Nobel" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Alfred Nobel kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.