Kizu

From Wikipedia

Kuzi
Kizu domo-njano
Kizu domo-njano
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Falconiformes (Ndege kama kozi)
Familia: Accipitridae (Ndege walio na mnasaba na mwewe)
Familia ndogo: Melieraxinae
Jenasi: Melierax
Gray, 1840
Spishi: Angalia katiba

Vizu ni ndege mbua wa jenasi Melierax ya familia Accipitridae. Mgongo na mabawa yao ina rangi ya kijivu na tumbo lao ni mweupe na milia kijivu. Spishi zote zinatokea Afrika kusini kwa jangwa Sahara. Zinapenda mahali pakavu kwenye miti. Hujenga tago lao kwa vijiti juu ya mti na hutaga mayai mawili au matatu, pengine yai moja. Wakati wa majira ya kuzaa huimba kwa milio ya mluzi. Hukamata wanyama na ndege wadogo na wadudu wakubwa.

[edit] Spishi

  • Melierax canorus Kizu Kusi (Pale Chanting Goshawk)
  • Melierax gabar au Micronisus gabar, Kizu Miguu-myekundu (Gabar Goshawk)
  • Melierax metabates, Kizu Domo-jekundu (Dark Chanting Goshawk)
  • Melierax poliopterus Kizu Domo-njano (Eastern Chanting Goshawk)

[edit] Picha