Kilwa Kivinje
From Wikipedia
Kilwa Kivinje ni mji mdogo katika Wilaya ya Kilwa ufukoni wa Bahari Hindi.
Wakati wa utawala wa Zanzibar ilikuwa makao ya liwali ya Sultani kwa ajili ya pwani la kusini la Tanzania ikichukua nafasi ya Kilwa Kisiwani kama mji muhimu katika sehemu hii ya pwani la kusini.
Ilikuwa makao makuu ya wilaya tangu zamani ya ukoloni wa Kijerumani. Tangu kuondoka kwa makao makuu ya wilaya mji umerudi nyuma. Nyumba za ghorofa za wafanyabiashara hazitumiki tena zimeanza kuporomoka. Boma la Kale la Wajerumani bado inatumika. Hospitali ya wilaya imebaki Kilwa Kivinje. Tarafa ina wakazi 13,374 (2002). Bandari ndogo inafaa jahazi tu .