Gelawdewos
From Wikipedia
Gelawdewos (takriban 1521 au 1522 – 23 Machi, 1559) alikuwa mfalme mkuu wa Uhabeshi kuanzia 3 Septemba, 1540 hadi kifo chake. Alimfuata Dawit II. Jina lake la kutawala lilikuwa Asnaf Sagad I. Utawala wake ulisumbuliwa hasa na vita. Kwanza alimpigia vita Ahmad ibn Ibrahim al-Ghazi aliyeshindwa na kufa katika mapigano yaliyofanyika mahali pa Wayna Daga, 21 Februari, 1543. Halafu alimpigia vita Nur ibn Mujahid aliyevamia Uhabeshi. Kuanzia mwaka wa 1557 Waturuki walipotwaa mji wa Massawa Gelawdewos alipata shida sana. Aliuawa katika mapigano dhidi ya Nur. Aliyemfuata ni Menas.