Injera
From Wikipedia
Injera ni aina ya chapati ambayo ni chakula cha asili ya Ethiopia, Eritrea na Somalia. Unga wa teff (nafaka ya pekee katika nyanda za juu za Ethiopia) huchanganywa na maji na kisha kuachwa hadi unapochacha baada ya siku chache. Baada ya hapo uji huo unakuwa tayari kupikia chapati. Injera huliwa na saladi au mchuzi uitwao Wat. Mchuzi huu huweza kuwa wa nyama ya ng'ombe au mbuzi. Kwakuwa unga wa Injera huwa umechacha, ladha yake huwa na uchachu.
Nje ya nyanda za juu watu wanatumia unga wa mchele, mahindi au nafaka nyingine ingawa kiasili ni teff.